logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Juma Jux aonekana na 'pacha' wa Vanessa Mdee kwenye ndege moja

Mwimbaji huyo pia alionyesha nyakati za kimapenzi kwenye ukurasa wake wa Instagram.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri17 January 2023 - 04:14

Muhtasari


•Jux alionekana akifurahia muda na mwanadada ambaye anafahamika kuwa Karen Bujulu, ambaye alichumbiana naye mwaka jana, na alikuwa video vixen wake.

•Wawili hao walikuwa wanaelekea Paris, mahali Juma Jux anapopenda kuenda likizo. 

Juma Jux ameonekana akiwa na mwanamke anayefanana sana na aliyekuwa mpenzi wake Vanessa Mdee.

Katika video iliyochapishwa kwenye mitandao ya kijamii, unaweza kumuona Jux akifurahia muda na mwanadada ambaye anafahamika kuwa Karen Bujulu, ambaye alichumbiana naye mwaka jana, na alikuwa video vixen wake.

Mwimbaji huyo pia alionyesha nyakati za kimapenzi kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Kwa upande wake Karen alinukuu picha ya ndege, "Wakati huu ninashika hisia na safari za ndege."

Wawili hao walikuwa wanaelekea Paris, mahali Juma Jux anapopenda kuenda likizo. Hata mashabiki wao walifurahi kwamba wawili hao wamerudi pamoja. Soma baadhi ya maoni hayo hapa chini;

tontofloxy...Msalimie jumaaa

dorice_8four..Mama Jux ingia paris

salazahke...Si ndio juma jux huyu hapa

lynee_mtandi...Kumbe upo na juma napenda couple yenu 😍😍

Katika video zilizofuata, Juma Jux alionesha amefika Ufaransa, huku akimuonyesha rafiki yake na eneo walilokuwa.

Pia walishiriki chakula cha jioni na tuliweza kuona kuna marafiki wengine, lakini hakugeuza kamera upande huo. Alionyesha tu rafiki wa kiume akiwa na chakula chake cha jioni cha kifahari.

Juma na Karen walivuma mitandaoni mwaka wa 2022 alipomtambulisha kama mwenza wake mnamo siku ya wapendanao, baadae iligeuka kuwa wimbo. Pia walienda likizo pamoja.

Karen ni mwanamke wa Kitanzania Mnyarwanda ambaye anapenda kusafiri na ana maudhui ya mazoezi ya mwili.

Jux basi wakati fulani aliacha ghafla kusambaza maudhui yake kwenye majukwaa yake, na kutuma ishara kuwa imekwisha. Muda mfupi baadaye, Huddah Monroe alianza kuonekana naye.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved