logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Wanaoeneza uvumi wa D poleni,'Mama Trio Mio ajibu madai ya msanii huyo kupata D

Alisema msanii huyo mashuhuri alifaulu katika mtihani huo uliotangazwa na Waziri Ezekiel Machogu.

image
na Radio Jambo

Habari20 January 2023 - 11:26

Muhtasari


  • Katika taarifa yake iliyoandikwa Ijumaa, Januari 20, Irma Sofia alieleza kuwa wengi wangesikitishwa na uvumi huo kuhusu mwanawe

Mamake msanii maarufu Trio Mio amekanusha madai kwamba mwanawe alipata D katika matokeo ya hivi punde ya 2022 yaKCSE.

Katika taarifa yake iliyoandikwa Ijumaa, Januari 20, Irma Sofia alieleza kuwa wengi wangesikitishwa na uvumi huo kuhusu mwanawe.

Alisema msanii huyo mashuhuri alifaulu katika mtihani huo uliotangazwa na Waziri Ezekiel Machogu.

Hata hivyo mama huyo hakufichua alichojizolea msanii huyo huku akisema kwamba anajivunia, matokeo ya mwanawe.

"Sitapumua kwa sababu matokeo ya KCSE yametangazwa? Tulia.

"Mvulana alifanya bora yake na ninajivunia sana. Na wale wanaobashiri D. Samahani!" soma taarifa hiyo kwa sehemu.

Kwa hiyo, baada ya kutoa taarifa hiyo msanii huyo aliweka sawa kwenye mitandao yake ya kijamii.

Sofia alikuwa akijibu baada ya madai kuwa msanii huyoalipata alama ya D kuibuka kwenye mitandao ya kijamii.

Ripoti hizo zilishuhudia msanii huyo akivuma kwenye mitandao ya kijamii huku baadhi ya Wakenya pia wakwazima waliokuwa wakimkejeli msanii huyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved