logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Bahati hatimaye afichua kwa nini alitoweka na kunyamaza baada ya kushindwa uchaguzi

Bahati ameweka wazi kwamba alichukua mapumziko kutoka kwa umma ili kuangazia muziki wake.

image
na Radio Jambo

Habari22 January 2023 - 06:10

Muhtasari


•Mwimbaji huyo ameweka wazi kwamba alichukua mapumziko kutoka kwa umma ili kuangazia muziki wake.

•Alibainisha kuwa ilikuwa ni mapumziko ya mitandao ya kijamii ya kwanza aliyokuwa akichukua katika kipindi cha miaka kumi

Mwanamuziki mashuhuri Kelvin Kioko almaarufu Bahati hatimaye amefunguka kuhusu ukimya wake punde baada ya uchaguzi wa Agosti 9, 2022.

Mwaka jana, msanii huyo mwenye umri wa miaka 30 alijitosa katika siasa na alikuwa mmoja wa wagombea kiti cha ubunge wa Mathare akiwania kwa tikiti ya chama cha Jubilee. Hata hivyo, alipoteza uchaguzi huyo kwa  mgombea wa ODM Anthony Oluoch.

Baada ya uchaguzi huo, Bahati alitoweka kwenye vyombo vya habari na mitandao yote ya kijamii huku Wakenya wengi wakikisia kuwa alikuwa amekumbwa na msongo wa mawazo kwa  kutofanikiwa kupata ushindi katika uchaguzi.

Mwanamuziki huyo hata hivyo ameweka wazi kwamba alichukua mapumziko kutoka kwa umma ili kuangazia muziki wake.

"Nilikuwa nimejifungia  tu kwenye Studio ya Nyumbani nikitengeneza Sauti Bora za Muziki kwa ajili yenu mashabiki wangu tangu siku ya kwanza," alisema kupitia ukuraa wake wa mtandao wa nstagram.

Alibainisha kuwa ilikuwa ni mapumziko ya mitandao ya kijamii ya kwanza aliyokuwa akichukua katika kipindi cha miaka kumi

"Naapa nasikiliza nyimbo ambazo nimepanga kuachia mwaka huu wa 2023 ata sina usingizi. Walai sikujua Bahati ni mkali hivii," alijigamba.

Bahati alidokeza kuwa umahiri wake katika muziki umeongezeka huku akifanya mzaha kuwa huenda imechangiwa na kuibiwa kwa kura zake.

Katika uchaguzi wa mwaka jana, Bahati aliibuka wa tatu katika kinyang’anyiro cha ubunge wa Mathare huku  Anthony Oluoch wa ODM akichukua ushindi. Billian Ojiwa ambaye aliwania kwa tiketi ya UDA alimaliza katika nafasi ya pili.

Hilo lilikuwa ni jaribio la Bahati la kwanza kuwania kiti cha kisiasa nchini Kenya.

Baada ya kuvunjwa moyo katika uchaguzi huo uliokuwa na ushindani mkubwa, mwanamuziki huyo alizama kwenye ukimya mrefu.

Hatimaye aliibuka tena hadharani baada ya takriban miezi miwili kwa wimbo  'Mambo ya Mhesh’ ambao alipakia kwenye YouTube.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved