logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Thomas Partey akejeliwa kwa kukubali kukunjwa mashati na Grealish, "umeangusha Waafrika!"

Kwa muonekano, Partey alikuwa makini asiiangushe timu kwa kupewa kadi nyekundu.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri29 April 2023 - 12:18

Muhtasari


• Wengi wanafahamu kwamba mwanamume mzima wa Kiafrika hawezi kukubali kukunjwa mashati kwa jinsi hiyo tena bila kulipa kisasi.

• Hii ndio falsafa iliyowatuma wengi kuhusi kwamba Partey kutoka Ghana aliisaliti faraja ya wanaume wa Kiafrika.

Jack Grealish akimkunja mashati vikali Thomas Partey.

Katikati mwa wiki hii, mechi ya kukata na shoka baina ya viongozi wawili katika jedwali la kigi kuu ya premia nchini Uingereza Arsenal na Manchester City ndio ilikuwa gumzo la mitaani.

Katika mechi hiyo ambayo ilikuwa inatajwa kuwa ya kuamua ubingwa wa ligi utaenda wapi kati ya viongozi Arsenal na wapinzani wa karibu City, kulikuwa na mihemko pamoja na mbwembwe za aina yake ambapo kila mchezaji kutoka pande zote mbili alikuwa anajitoa kwa jino na ukucha kuhakikisha kwamba hakosei na kubeba lawama ya matokeo baada ya dakika tisini.

Tukio moja ambalo limebaki kuwa gumzo mitandaoni ni lile lililowahusisha viungo, Mghana Thomas Partey wa Arsenal na Muingereza Jack Grealish wa Manchester City.

 Katika picha ambazo zimeenea mitandaoni, Grealishi alionekana amemkunja mashati Partey kiasi kwamba alimkaba hadi kwenye koo huku maskini Partey akiwa amebabi katika kumuangalia kwa macho ya huruma aitegemea msamaha.

Tukio hilo limezua mjadala baadhi ya wanamitandao wa Kiafrika wakihisi kwamba Partey aliwaangusha kwani kitamaduni mwanamume mzima wa Kiafrika hawezi kubali kukunjwa mashati hivyo, kwani bora zichapwe tu!

“Partey ameangusha Waafrika kwa kukubali Grealish kumkunja mashati hivi bila kujibu mipigo,” mmoja kwa jina Albert Nat Hyde aliandika kwenye ukurasa wa Twitter.

“Partey amewaangusha Waafrika kwa kumruhusu Grealish kumnyakua hivi bila kulipiza kisasi. Huwezi kufanya hivi kwa Sadio Mane au hata Iheanacho. Partey ana kazi ya kufanya.” Mwingine alisema.

Lakini kutokana na uhalisia wa maneno na jinsi hali ilivyokuwa, Partey alionekana kuwa makini sana kutojibu fujo za Grealish kwani hakutaka kuiangusha timu yake kwa kurambishwa kadi nyekundu.

Wewe unasemaje kuhusu tukio hilo lililoshuhudiwa uwanjani Etihadi Jumatano ya Aprili 26?

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved