logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msanii Ray C yuko tayari kupata mtoto wa 2,miezi chache baada ya kumkaribisha kifungua mimba

Ray C alimkaribisha mtoto wake wa kwanza ulimwenguni katikati ya Februari 2023.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri13 June 2023 - 11:42

Muhtasari


  • Ray C alifichua hayo kupitia kipande cha video alichoshiriki kwenye hadithi zake za Instagram, alipokuwa kwenye duka fulani la nguo lililokuwa likiuza nguo za watoto wa kike.
Ray C

Staa mkongwe wa Bongo Flava, Rehema Chalamila maarufu kwa jina la Ray C yuko tayari kupata mtoto wa pili, baada ya kumkaribisha mtoto wake wa kwanza miezi michache iliyopita.

Mwimbaji huyo mashuhuri mwenye umri wa miaka 41 tayari ameweka ratiba ya lini hilo litafanyika, pamoja na jinsia ambayo anapendelea kwa mzaliwa wake wa pili.

Ray C alifichua hayo kupitia kipande cha video alichoshiriki kwenye hadithi zake za Instagram, alipokuwa kwenye duka fulani la nguo lililokuwa likiuza nguo za watoto wa kike.

Aliiambatanisha zaidi na nukuu inayosema kwamba sasa anataka binti, ambaye anatarajia kuwa naye mwaka ujao.

“KUOMBEA MSICHANA MWAKA UJAO HEHE” Ray C aliandika.

Ray C alimkaribisha mtoto wake wa kwanza ulimwenguni katikati ya Februari 2023.

Msanii huyo kutoka Tanzania alimkaribisha mtoto wa kiume na mpenzi wake, na akamwita Shah Rukh.

Akitangaza habari njema kisha alishiriki picha ya mtoto mchanga, na akaisindikiza na nukuu inayosema:

"Naitwa mama Shahrukh".

Mwanamuziki huyo alifichua ujauzito wake mnamo Februari 7, na kuelezea jinsi alivyojitahidi kuuweka siri.

Kwenye ukurasa wake wa Instagram, Ray C alichapisha video iliyoonyesha tumbo lake likiwa limechomoza sana.

"Wakati wa Mungu ni wakati sahihi," aliandika chini ya video hiyo.

Mwimbaji huyo kwa sasa anaishi na mume wake mzungu nchini Ufaransa. Alihamia nchi hiyo ya Ulaya miaka michache iliyopita na kwa muda mrefu amekuwa akiweka maisha yake ya kibinafsi kuwa siri.

Shahrukh ni mtoto wa kwanza wa Ray C. Takriban miaka minne iliyopita alifunguka kuhusu ujauzito wake kuharibika.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved