Watoto wangu hawakumpenda mume wangu Shakib walipokutana naye mara ya kwanza-Zari

Akijibu swali la iwapo anamtunza kifedha, Zari alisema kikubwa ni kuleta amani na kumfurahisha.

Muhtasari
  • Tafrija haikuenda kama ilivyotarajiwa kwani Zari na promota walijibizana hadharani kuhusu tukio hilo kufeli.
  • Promota huyo alivujisha sauti ya Zari akimkosoa mumewe Shakib Luutaya kwa kukosa uzoefu wa kusafiri kimataifa.
Shakib na Zari
Image: INSTAGRAM// SHAKIB

Zari Hassan Luutaya yuko nchini kwao Uganda.Mfanyabiashara huyo hajaonekana hadharani na mumewe tangu safari yao ya kwenda Uingereza mwishoni mwa Juni.

Tafrija haikuenda kama ilivyotarajiwa kwani Zari na promota walijibizana hadharani kuhusu tukio hilo kufeli.

Promota huyo alivujisha sauti ya Zari akimkosoa mumewe Shakib Luutaya kwa kukosa uzoefu wa kusafiri kimataifa.

Alimwita mpumbavu na mwanaume asiyejiamini. Lawama zilizompata Zari zilikuwa kali huku wanamtandao wakimchukulia poa kwa kumkejeli mpenziwe.

Alijaribu kutetea maoni yake alipokuwa akienda kwenye mtandao wake wa kijamii kuzungumza juu ya kuwa mpumbavu wa mapenzi.

Katika mahojiano ya kipekee na Mwasuze Mutya wa NTV Uganda Jumatatu, Julai 10, Zari alifafanua maoni yake ya awali wakati huohuo akimsifu.

"Nilitaka Lutaaya awe pamoja nami Uingereza na ni vigumu kupata VISA kwa hivyo chochote nilichosema hakikuwa na nia ya kumuaibisha au kumvunjia heshima mume wangu. Wanawake huzungumza kuhusu waume zao faraghani, ni upuuzi mtu ambaye nilidhani ni rafiki yangu alinisaliti,” alisema.

Alimwita jasiri kwa kumchumbia,

"Sherehe ya Nikah ilikuwa ya kushtukiza. Yeye kwa kushirikiana na marafiki wachache waliandaa ndoa. Sikusita kwa sababu nilimpenda. Ujasiri wake ulinishtua tu, sikutarajia angeondoa hatua kama hiyo.

Niliomba Quran kwa Mahr (mahari). Mume wangu Lutaaya alikuwa na maisha yake kabla hatujaonana. Anafanya kazi na kama mtu mwenye shughuli nyingi, hata baada ya kufunga ndoa, hatuko pamoja kila wakati. Anakuja anapopata muda au nikiwa huru. Watu walianza kumfahamu kupitia mimi,”

Pia alisema yeye ni mnyenyekevu na humfurahisha.Pia alisema yeye ni mwanamume anayeomba sana ambaye ana mazoea ya kumpigia simu na kumkumbusha kufanya hivyo.

"Niliomba Quran kama Mahr (mahari) kwa sababu niko katika safari ya kiroho na Allah. Mume wangu, Shakib huomba sana kwa hivyo ninahisi hatia nisipofanya hivyo na huwa ananipigia simu kunikumbusha kusali wakati hayupo,” Zari alisema.

Anafichua kuwa familia yake haikuidhinisha uhusiano huo, lakini walimpa baraka zao bila kujali.

"Watoto wangu hawakukubali uhusiano wangu na Shakib lakini baada ya kushuhudia jinsi tulivyokuwa karibu na tukiwa na furaha, walimwomba ahakikishe kwamba ananitunza vizuri."

Akijibu swali la iwapo anamtunza kifedha, Zari alisema kikubwa ni kuleta amani na kumfurahisha.