logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Tanzia! Tasnia ya Bongo katika maombolezo kufuatia kifo cha mwimbaji Haitham Kim

Marehemu alikuwa amekumbwa na matatizo ya kupumua na kupelekea kulazwa.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri01 September 2023 - 11:21

Muhtasari


•Marehemu amekuwa akipokea matibabu maalum katika hospitali ya Rufaa ya Temeke jijini Dar es Salaam baada ya kupata matatizo ya kupumua.

Mwimbaji wa Bongo Fleva Haitham Kim ameaga dunia.

Kim ambaye katika siku za hivi majuzi amekuwa akipokea matibabu maalum baada ya kupata matatizo ya kupumua aliaga dunia katika hospitali ya Rufaa ya Temeke jijini Dar es Salaam, mwendo wa saa sita mchana siku ya Ijumaa.

Marehemu amemuacha nyuma mtoto wake mmoja.

Haya yanajiri siku chache tu baada ya wasanii wa Bongo kuanzisha kampeni ya kuchangisha pesa kwa ajili ya matibabu yake ya gharama.

Inaripotiwa kuwa marehemu alikuwa amekumbwa na matatizo ya kupumua ambapo ilianza kama homa ya kawaida lakini baadaye akawa anakosa pumzi hadi kulazwa.

Mashabiki, marafiki, wanafamilia na watu wengine wa karibu wameendelea kumuomboleza mwimbaji na mwandishi huyo wa nyimbo.

Nandy ni miongoni mwa mastaa ambao wamemuomboleza kwa ujumbe wa kihisia.

“Mungu atupe mwisho mwema @haithamkim. Jamani mdogo sana poleni ndugu, jamaa na marafiki kwa ujumla. Hili ni pigo tasnia. Pumzika kwa amani mama,” aliomboleza Nandy.

Zuchu, Kajala Masanja, Hamisa Mobetto, Mr Seed na Wema Sepetu ni miongoni mwa wasanii wengine ambao wamemuomboleza mama huyo wa mtoto mmoja.

Mungu ailaze roho ya Kim pema peponi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved