logo

NOW ON AIR

Listen in Live

YouTube yafunga akaunti ya Mwanablogu Andrew Kibe

Kibe aliwataka mashabiki wake wawe na subira kwa jukwaa jipya.

image
na

Habari12 September 2023 - 05:56

Muhtasari


•Andrew Kibe amelazimika kufanya mabadiliko  makubwa baada ya kurasa wake wa Youtube wenye  mashabiki zidi ya  elifu mia inne (400 K) wanaommfuatilia kufungwa .

•Aliweka wazi kuwa haungi mkono hatua zilizochukuliwa na mtandao huo dhidi yake, 

Muunda maudhui wa Marekani, Andrew Kibe.

Mwana  blogu Andrew Kibe amelazimika kufanya mabadiliko  makubwa baada ya kurasa wake wa Youtube wenye  mashabiki zaidi ya  laki nne wanaommfuatilia kufungwa.

Japo Kibe hakueleza sababu zilizopelekea akaunti yake kufungwa, alitoa maelezo kuhusu hatua hiyo ya Youtube kwa mashabiki wake.

Aliwarai mashabiki wake wawe wenye subira na waaminifu kwani kuna jukwaa jipya ambalo maudhui yake yatatiririshwa.

Aliweka wazi kuwa haungi mkono hatua zilizochukuliwa na mtandao huo dhidi yake, ila alisema ana matumaini kuwa atarejea mtandaoni kwa njia zozote zile.

Katika ujumbe aliochapisha kwenye kurasa zake alisema;

"Nipate usiku wa leo kwenye, X, Rumble,Instagram, na Tiktok."

Mashabiki wake walishangazwa kuona kwamba kurasa za Andrew kibe zimesimamishwa kufuatia madai ya kukiuka kanuni na masharti ya mtandao huo.

"Akaunti ya Youtube inayohusishwa na video hii imesitishwa,"

Awali Kibe alikua amchapisha video kwenye mitandao akimkmea vikali kijana mmoja  mfanyibiashara ambaye alilazimia kufunga biashara zake za kuuza mayai ya kuchemshwa ili kuendelea na masomo yake, jambo ambalo Kibe alilichukulia kuwa ni la kupoteza muda.

Kulingana na sheria za Google zenye uwezo wa kusimamisha akaunti zinasema kuwa;

Iwapo kituo chako kilikatishwa kwa sababu ya madai ya  ukiukaji wa hatimiliki na unahisi madai hayo si sahihi, unaweza kuwasilisha arafa ya kukanusha. Ila fomu ya wavuti ya arafa ya kukanusha haitapatikana.

Hili linatia shaka kwa mwanablogu huyo kwani Youtube inaweza kusimamisha akaunti kwa muda au kabisa.

Kibe amejibu madai haya katika ukurasa wake wa Tiktok akisema kuwa bado angali imara kwa kazi zake na kuhakiki kuwa hatua zilizochukuliwa hazitamzuia kutoa huduma zake.

Cha kutia moyo kwa Mwanablogu huyu sasa ni kuwa, mashabiki wameahidi kumfuata katika mtandao wowote ule ili kupata huduma zake.

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved