logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kate Actress awajibu mashabiki wanaojulia hali baada ya kutengana na mumewe

Kate Actress alikuwa mwenye furaha kutokana jumbe hizo na kumjulia hali.

image
na

Habari21 September 2023 - 12:15

Muhtasari


• Ujumbe wa Kate Actress kwa mashabiki na wafuasi wanaopiga simu na kutuma jumbe kwenye simu yake baada ya kutengana na Phil ulikuwa shukrani.

• Wapenzi hao wawili walitoa taarifa ya pamoja Jumanne, Septemba 19, 2023, wakisema kwamba ndoa yao ilivunjika muda mfupi uliopita lakini na wakachagua kuweka  mambo yao faragha.

mwigizaji Kate

  Mwigizaji Catherine Kamau almaarufu Kate Actress ameandika ujumbe wa shukrani kwa mashabiki na wafuasi wake siku chache baada ya kutangaza kutengana na mpenzi wake Phillip Karanja.

Katika ujumbe wake, Kate alitoa shukrani kwa kila mtu ambaye alikuwa amemtumia ujumbe au kumpigia simu kuulizia jinsi anavyoendelea na maisha.

"Asante sana kwa jumbe zenu ninazipokea kila siku  pia jumbe zenye nazipata kila wakati asanteni sana" Kate alisema.

Ujumbe wa shukrani unakuja siku chache baada ya mwigizaji huyo wa zamani wa kipindi  Mother-In-Law kufichua kwamba aliachana na mume wake Phillip Karanja kwa amani.

Phillip Karanja pia alijiunga na mazungumzo hayo kuthibitisha kwamba kwa hakika wametengana  na watu wanapaswa kuwaruhusu waendelee na maisha yao tofauti.

"Hii ni Mambo ya Watu wawili, lakini turuhusu tu iwe hivo ili tuendelee na maisha yetu bila maswali mengi," Phil alisema.

Aliongeza kuwa wanabaki kuwa marafiki; "Mimi na Kate tunabaki kama marafiki, Wazazi wenza na washirika wa biashara,".

Wawili hao walikuwa wameoana kwa zaidi ya miaka mitano sasa na wana binti mmoja pamoja.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved