Pasta T Mwangi asema kwa nini wanaume hawafai kulipa mahari

Dhana ya kulipia wanawake mahari ni utumwa ni jambo limepitwa na wakati

Muhtasari

•Mbona wanawake wabadilishwe na dhamana ya chini kama Mbuzi jambo linawakosea heshima ndio sababu napinga kulipwa kwa mahari

Image: Pasta T.Mwangi

Mhubiri wa  kanisa la Life Church International Mchungaji T. Mwangi anapinga mila ya wanaume kulipa mahari kwa mwanamke anayenuia kuoa.

 Baada ya wanablogu wa mitandao ya kijamii kutembelea mchugaji huyu kwa mahojiano ya moja kwa moja  Kulingana na Mchungaji T wanaume wanafaa kujadiliana na wazazi wa  wote ili kuafikiana lakini sio kulipa mahari.

 

"Dhana ya  mahari ya kununua mwanamke ndio awe mke wako  hufanya Mwanamke kukosa thamani kwa sababu mwanaume atakuwa na fikra  baada ya kulipa mahali amemumiliki. Jambo hili litafanya mwanamke kukosa haki kwa familia, halifai kwa sababu wanawake watalinganishwa na chombo chochote cha kununua pale nyumbani, mbona wazazi                                               wauze mtoto wao". alisema .

Mchungaji huyo alizidi kusema Wanaume hujiuliza maswali mengi wakati wa mkutano wa kulipia wanawake mahari  kwa mfano wazazi wa mwanadada anayetaka kuolewa wanaweza  kutaka Mbuzi au Ng'ombe kumi na kiasi cha pesa kama elfu kumi, jambo ili linaweza kuleta fikikra kwa akili ya mwanaume...kumfananisha mwanamke huyo kuwa wa thamani ya chini .

Alieleza kuwa ni aina ya utumwa, ambapo mwanamume hulipa pesa ili mwanamke awe mke wake.

Hapo awali  Mchungaji T alisema hakumlipia mahari mkewe hata baada ya wakwe wachache kumlazimisha kufanya hivyo na hata kutuma wazee kuzungumza naye.