logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kisa cha aibu wakati makalio bandia ya mrembo yalianguka akiwa ananengua jukwaani (Video)

Video ya tukio hilo imezua vichekesho na maoni kinzani kutoka kwa watu.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri03 November 2023 - 05:47

Muhtasari


• Pindi alipoingia jukwaani na kuanza kucheza densi, mwanamume mmoja alimkaribia na kumuomba kucheza densi pamoja.

Makalio feki

Mwanamke mmoja mrembo alisalia na kovu la aibu la kudumu katika nafssi yake baada ya tukio la aibu kumfika akiwa katika kbalu cha starehe akipunja raha.

Kwa mujibu wa video ya tukio hilo ambayo imeenezwa pakubwa kwenye mitandao ya kijamii, mrembo huyo mwenye umri wa makamo alijitoma kwenye jukwaa wakati DJ aliweka muziki wake pendwa.

Alikuwa amevalia rinda la njano lililomchora vizuri maungo yake, lakini wengi hawakuwa wanajua kwamba makalio yale aliyokuwa nayo hayakuwa halisi bali ni ya kughushi tu.

Pindi alipoingia jukwaani na kuanza kucheza densi, mwanamume mmoja alimkaribia na kumuomba kucheza densi pamoja kufurahia muziki wa mapenzi.

Ghafla densi ikiwa imeshika kasi makalio feki ya mrembo yule yaliporomoka na kutawanyika kwenye sakafu ya kucheza densi na kuwaacha watu waliojaa katika klabu hicho kwa vicheko vya kustaajabu.

Video ya tukio hilo imezua vichekesho na maoni kinzani kutoka kwa watu huku wengi wakishauri kina dada kujisitiri kwa njia halisi ili kuepuka visa vya aibu kama hivyo.

Tazama video ya tukio hilo hapa chini.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved