logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Kamene Goro azungumzia madai ya ujauzito, aeleza sababu ya shida yake ya kutembea

Kamene amepuuzilia mbali tetesi za ujauzito ambazo zimekuwa zikienezwa kwenye mitandao ya kijamii katika siku za hivi majuzi.

image
na Radio Jambo

Habari01 April 2024 - 05:33

Muhtasari


•Kamene amepuuzilia mbali tetesi za ujauzito ambazo zimekuwa zikienezwa kwenye mitandao ya kijamii katika siku za hivi majuzi.

•Alizungumzia jinsi ambavyo amekuwa na safari ngumu ya kupona, akibainisha kuwa amekuwa akitembea kwa magongo kwa muda mrefu.

Kamene Goro/

Aliyekuwa mtangazaji wa redio, Kamene Goro amepuuzilia mbali tetesi za ujauzito ambazo zimekuwa zikienezwa kwenye mitandao ya kijamii katika siku za hivi majuzi.

Katika taarifa yake ya  Jumapili, mrembo huyo mwenye umri wa miaka 32 alibainisha kuwa kumekuwa na ripoti nyingi za ujauzito ambazo zimeibuka kutokana na mtindo wake wa kutembea.

Video ambazo zilichukuliwa wakati wa kusherehekea siku yake ya kuzaliwa siku kadhaa zilizopita zikimuonyesha akihangaika kutembea zimekuwa chimbuko la uvumi huo.

"Katika wiki iliyopita nimeona maoni mengi, uvumi kuhusu jinsi nilivyokuwa nikitembea kwenye siku yangu ya kuzaliwa, na kila mara inarudi kwenye hitimisho lile lile la kizamani la kutojali kwamba mimi ni mjamzito. Jameni, nilisema sitawahi kujibu lakini ninahisi ninafaa kwa sababu maoni hayo hayana msingi na ni ujinga,” Kamene Goro alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Huku akieleza sababu ya shida lake la kutembea, mtangazaji huyo wa zamani wa redio alibainisha kuwa ni athari za upasuaji wa goti aliofanyiwa mapema mwaka huu.

Kamene alizungumzia jinsi ambavyo amekuwa na safari ngumu ya kupona, akibainisha kuwa amekuwa akitembea kwa magongo kwa muda mrefu.

"Kumbuka Januari nilifanyiwa upasuaji kwenye goti ambalo liliniweka hospitalini kwa siku 5. Sijatembea kwa muda mrefu, ni katika kuelekea siku yangu ya kuzaliwa ambapo nilianza kujaribu kutembea bila magongo yangu,” alisema.

Aliongeza, "Ni mchakato mgumu kujaribu kurejesha shughuli na nguvu ya misuli kwenye goti, ndiyo sababu ninatembea au kutembea kwa njia ya kuchekesha. Ni ahueni ngumu sana kwa uaminifu."

Kufuatia tetesi za ujauzito wa hivi majuzi, mke huyo wa Deejay Bonez sasa amewataka watumiaji wa mtandao kufanya uchunguzi wa kina  kila mara na kuuliza kabla ya kufanya hitimisho.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved