logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mchungaji Kanyari akabidhiwa kondomu, arimis kama zawadi wakati wa ibada kanisani

Mchungaji Kanyari alikabidhiwa Kondomu na tiktoker ya kike wakati wa Ibada ya Jumapili

image
na

Habari20 May 2024 - 08:41

Muhtasari


•TikToker Faith Peters alimzawadia mhubiri huyo mwenye utata zawadi tatu, miongoni mwao ikiwa ni pakiti ya mipira ya kondomu, kabla ya kukiri kumpenda.

•Vitendo vya Faith vilizua hisia tofauti kwa wanamtandao, huku baadhi wakimlaumu kwa kutoliheshimu Kanisa.

MCHUNGAJI VICTOR KANYARI

TikToker wa kike aliyetambulika kwa jina la Faith M Peters aliwaacha wengi kwa mshangao baada ya kufika kanisani kwa Mchungaji Kanyari na kumzawadi mhubiri huyo zawadi tatu moja wapo ikiwa pakiti ya kondomu.

Mfanyabiashara huyo alimpa Kanyari kifurushi kidogo kilichokuwa kimefungwa kwenye gazeti. Alipofungua, Kanyari, ambaye alikuwa amesimama kwenye madhabahu, alionyesha  vitu hivyo tatu: kotex  liner, arimis petroleum jelly na pakiti ya kondomu.

Faith kisha alikiri kuwa aliota kuwa yeye na Kanyari walikuwa na harusi kubwa. Mwanamke huyo jasiri alibaini kuwa alifahamu kuwa wanawake wengi walikuwa wakipenda mapenzi ya Kanyari, na akamshauri kutumia kinga.

"Naona wanawake wanataka sana Pastor Kanyari, nimkuletea kinga ya maisha. Tumia kinga baba, usikatae wanawake," alisema.

 Faith alidai kumpenda mhubiri huyo mwenye utata, akimsihi amuoe.

 “Nataka utoke pale kwa Rish Kamunge kuja hapa. Watoto zaidi kwa hawa watoto wa Marekani tutaongeza nimechoka," alisema.

Vitendo vya Faith vilizua hisia tofauti kwa wanamtandao, huku baadhi wakimlaumu kwa kutoliheshimu Kanisa.

Monique's Danielson :

     "Eiish mnaeenda spidi sana. Hamuogopi hata man of God.

Mercy Mutuli :

   "Ooh God, have mercy upon us."

 Ngetich Langat Jeff :

    "That was the best gift ever been awarded ."

Festus Murithi Poul :

   "Condom kwa kanisa ?? Pastor yawa."

 Pappa Samwely Comedian :

   "The lady may be signifying something about."

Shiku Philip :

      "This is too much."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved