logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ndege iliyombeba makamu wa rais wa Malawi yatoweka

Ndege iliyokuwa imembeba Makamu wa Rais wa Malawi Saulos Chilima na watu wengine tisa imetoweka.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku11 June 2024 - 03:54

Muhtasari


•Ndege ya Jeshi la Ulinzi la Malawi "ilitoweka kwenye rada" baada ya kuondoka katika mji mkuu, Lilongwe, Jumatatu asubuhi, taarifa hiyo iliongeza.

•"Wananchi wataarifiwa kuhusu maelezo yoyote kuhusu hali hiyo ukweli unapothibitishwa," ofisi ya rais ilisema.

Ndege iliyokuwa imembeba Makamu wa Rais wa Malawi Saulos Chilima na watu wengine tisa imetoweka, taarifa kutoka ofisi ya rais imesema.

Ndege ya Jeshi la Ulinzi la Malawi "ilitoweka kwenye rada" baada ya kuondoka katika mji mkuu, Lilongwe, Jumatatu asubuhi, taarifa hiyo iliongeza.

Rais aliamuru operesheni ya utafutaji na uokoaji baada ya maafisa wa anga kushindwa kuwasiliana na ndege hiyo.

Ilitakiwa kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mzuzu, kaskazini mwa nchi hiyo, baada ya saa 10:00 kwa saa za huko (11:00 BST)

Baada ya kuambiwa tukio hilo na kamanda wa Jeshi la Ulinzi, Rais wa Malawi Lazarus Chakwera amefuta safari yake ya kuelekea Bahamas.

"Wananchi wataarifiwa kuhusu maelezo yoyote kuhusu hali hiyo ukweli unapothibitishwa," ofisi ya rais ilisema.

Sababu ya kutoweka kwa ndege hiyo bado haijajulikana, Jenerali Valentino Phiri alimweleza Bw Chakwera. Moses Kunkuyu, waziri wa habari wa Malawi, aliiambia BBC kuwa juhudi za kutafuta ndege hiyo ni "kubwa".

Bw Chilima alikuwa akielekea kuiwakilisha serikali katika mazishi ya waziri wa zamani Ralph Kasambara, aliyefariki dunia siku tatu zilizopita.

Kabla ya taaluma yake ya kisiasa, alishikilia nyadhifa muhimu za uongozi katika kampuni za kimataifa kama Unilever na Coca Cola.

Bw Chilima, mwenye umri wa miaka 51, amekuwa makamu wa rais wa nchi hiyo ya kusini mwa Afrika tangu 2014.

Ameoa na ana watoto wawili.

Tutaendelea kukuletea taarifa zaidi kadiri tutakavyozipata.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved