Nelly anaomba watoto 4- Akothee azungumzia familia ya ndoto ya mpenzi wake

Wapenzi hao wamekuwa wakichumbiana kwa muda mrefu ila bado hawana mtoto pamoja.

Muhtasari

•Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 43 alidai kuwa mpenziwe anataka angalau watoto wanne, huku mmoja akiitwa Elizabeth Uganda Okuna.

Image: INSTAGRAM// AKOTHEE

Msanii na mjasiriamali maarufu wa Kenya Esther Akoth almaarufu Akothee amefichua familia ya ndoto ya mpenzi wake, Nelly Oaks.

Kwa siku chache zilizopita, wapenzi hao wawili wamekuwa katika ziara ya kikazi nchini Uganda ambapo wamepata nafasi ya kuzuru maeneo kadhaa ya nchi hiyo jirani, kukutana na watu mashuhuri pamoja na mashabiki.

Katika mojawapo ya machapisho yake ya matangazo, mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 43 alidai kuwa mpenzi wake anataka angalau watoto wanne, huku mmoja akiitwa Elizabeth Uganda Okuna.

“Yooo Uganda, Tumefanya upya viapo vyetu tayari.  Ardhi ya mahaba na utulivu.  Ona hewa safi za ndege,” Akothee aliandika chini  ya picha zake na Nelly Oaks alizochapisha Ijumaa,

Aliongeza, "Nelly anaomba watoto 4 na badomtoto  nambari moja ni kupanda tu 🤣🤣🤣🤣🤣. Nelly anasema mtoto wake ataitwa Elizabeth Uganda Okuna 🇺🇬. Yawaaa.”

Wawili hao wamekuwa wakichumbiana kwa muda mrefu sasa, hata hivyo wameachana na kurudiana mara kadhaa.

Mwezi uliopita, Akothee mpenziwe ambaye pia ni meneja wake alipokuwa akiadhimisha siku yake ya kuzaliwa na kutumia fursa hiyo kufunguka kuhusu jinsi wanavyopendana.

Akothee alizungumzia jinsi ambavyo bado wamejipata pamoja licha ya kujaribu kuachana katika siku za nyuma na hata kujaribu mahusiano mengine.

"Kheri ya siku ya kuzaliwa osiepna. Osiepnani bende oseyuare koda ndi. Wanafiki ,josem , tumejaribu kuwachana, tuka kimbia tukajaribu kwingine, sote tulikosa amani huko tumerudi," Akothee alimwandikia Nelly Oaks kupitia mtandao wa Instagram.

Aliongeza, "Hatujui jinsi ya kuachana. Tunachojua ni jinsi ya kurudi pamoja. Nadhani sisi sote ni SUMU 🤣🤣🤣. Hii ndiyo maana halisi ya uhusiano wenye sumu.”

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 43 aliendelea kuwaonya wale wanaojaribu kuchumbiana naye au Nelly Oaks baada ya kutengana, akiwasihi wasiwe na raha katika uhusiano huo kwani kuna uwezekano wa wao kuachwa wakati wowote.

"Ikiwa utaingia kwenye uhusiano na yeyote kati yetu ndani ya miezi 6 ya mapumziko yetu, usitulize kichwa chako hapo. Siku tukikutana kwenye tamasha au popote pale, utawachwa kwa mataaaaaa. Sisi pia hatujui kwanini? Hatuhoji hata kilichotokea,  baadhi yetu tulipiga hatua kubwa kwa kuwa msichana mkubwa, kiliniramba kweli kweli 🤣🤣🤣," alisema.

Pia alitangaza kwamba hatagura uhusiano na meneja wake tena, hata wakati kutoelewana kunatokea.

"Sasa sitaita kutokuelewana kwetu kuwa ni kuvunjika, nitajaribu kufanyia kazi uelewa wetu mdogo ikiwa kutoelewana hakufanyi kazi. Safari hii, sipangi virago, nitaenda naye. Madam Pack na usiende mahali popote. Mapenzi niue. Kijana ni wangu. Shoneni vitenge,” alisema.

Akothee alirudiana na mwanamume huyo ambaye pia ni meneja wake, katikati mwa mwaka jana, miezi michache tu baada ya ndoa yake na Denis Schweizer kuvunjika