logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa ahukumiwa mwezi 1 jela kwa kunusa viatu vya jirani

Mlalamishi alieleza korti ya Thessaloniki kuwa tabia hiyo ilikuwa inamkosesha amani.

image
na Brandon Asiema

Dakia-udaku22 October 2024 - 11:41

Muhtasari


  • Jamaa huyo mwenye umri wa miaka 28 alishindwa kujitetea kwa kueleza tabia yake ya kunusa viatu vya jirani zake japokuwa alisema tabia hiyo imemtia aibu kubwa sana.
  • Mahakama imeamuru jama huyo kuhudhuria vikao vya matibabu ili kupata usaidizi mwafaka

Mahakama moja nchini Ugiriki, imemhukumu kifungo cha mwezi mmoja jela jamaa mmoja aliyedaiwa kuwakosesha jirani zake amani kwa kupenyeza mara kwa mara kwa boma lao na kunusa viatu.

Akiwa mbele ya korti ya Thessaloniki, jamaa huyo mwenye umri wa miaka 28 alishindwa kujitetea kwa kueleza tabia yake ya kunusa viatu vya jirani zake japokuwa alisema tabia hiyo imemtia aibu kubwa sana.

Mshukiwa huyo alikiri kuwa hakuwa na nia ya kuvunja sheria wala kumdhuru mtu yeyote katika kutekeleza kosa hilo la kuwakera jirani zake na kwamba hakufahamu ni kwa nini alikuwa anatekeleza kisa hicho.

Hata hivyo walalamishi waliiambia korti kuwa jamma huyo hakuonyesha ishara yoyote ya uchokozi wakati wa ziara zake za usiku katika boma lao.

Mshukiwa huyo alikamatwa na polisi akiwa mbele ya  nyumba ya mlalamishi akinusa viatu vilivyokuwa vimewachwa nje usiku mmoja baada ya mlalamishi kujulisha polisi kuhusu kisa hicho.

Mahakama ya Thessaloniki iliambiwa kuwa kulikuwepo visa zaidi ya mara tatu vya jamma huyo kukosesha jirani zake amani katika muda wa miezi sita iliyopita licha yawalalamishi kutoa taarifa kwa familia ya mshukiwa kutaka kumkomesha.

Tatizo hilo lilikadiriwa kumalizikia mahakamani baada ya walalamishi kukosa kupata suluhu kufuatia malalamishi yao kwa familia ya mshukiwa.

Hata hivyo, mshukiwa atatakiwa kuhudhuria vikao vya matibabu ilikupata ushauri nasaha wa kurekebisha tabia hiyo iliyomweka mashakani.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved