logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Huddah awashauri Wakenya kuwapa sapoti watengenezaji wa samani nchini.

Mwanashoshalaiti huyo alijutia kununua kochi kutoka Dubai kwa bei nafuu kisha usafirishaji ukawa bei ghali

image
na Brandon Asiema

Dakia-udaku11 November 2024 - 11:26

Muhtasari


  • Wakati wa kuisafirisha Kenya, Huddah amesema kuwa alijutia kiwango cha fedha alizolipa kwani kochi hiyo ilichukua nafasi yote ya mita za ujazo yaani cubic meter na kulipia shilingi elfu sitini na tano.
  • Huddah alisisitiza kuwa ikiwa si kitu cha kipekee ambacho hakipatikani Kenya, aliwataka Wakenya kuwacha kununua samani kutoka nchi za nje.

caption

Mwanashoshalaiti Huddah Monroe amewashauri Wakenya wanaoagiza samani kutoka nchu za ughaibuni kuwacha kununua makochi kutoka nchi za nje na badala yake kununua samani kutoka kwa wafanyabiashara na fundi wanaotengeza bidhaa hiyo humu nchini.


Huddah amesema kuwa kitu kibaya sana unaweza kuagiza kutoka nchi za ughaibuni ni samani akiashiria kuwa unaweza dhani ni bei nafuu kumbe sivyo.


Kwa mujibu wa Huddah, samani inaweza kuchukua shehena moja ya usafirishaji wa mizigo kuingia ndani ya nchi ambayo inagharimu kati ya shilingi elsfu sitini na elfu sitini na tano.


Mwanashoshalaiti huyo amejutia namna aligharamika kuagiza samani kutoka nchi ya nje badala ya kumpiga sapoti rafiki wake aliyekuwa na bidhaa sawia na ile aliyokuwa ameagiza. Huddah amesema kuwa alinunua sofa moja kutoka Dubai kwa Dirham 1000 sawia na shilingi takribani 35,000 za Kenya akidhania ni bei nafuu.


Wakati wa kuisafirisha Kenya, Huddah amesema kuwa alijutia kiwango cha fedha alizolipa kwani kochi hiyo ilichukua nafasi yote ya mita za ujazo yaani cubic meter na kulipia shilingi elfu sitini na tano.


Mwanashoshalaiti huyo aidha amewataka Wakenya kuwacha kuagiza samani kutoka ughaibuni.


“Ujinga kamili. Nunua samani kutoka kwa watu wa nyumbani. Sofa huuzwa ata shilingi 55,000.” Aliandika Huddah Monroe kwa ukurasa wake wa Instagram.


Vile vile, Huddah alisisitiza kuwa ikiwa si kitu cha kipekee ambacho hakipatikani Kenya, aliwataka Wakenya kuwacha kununua samani kutoka nchi za nje.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved