logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mhubiri James Ng'ang'a awaonya wenye rasta dhidi ya kuhudhuria kanisa lake

“We kama uko na rasta nyoa, utanyoa. Ukija mahali niko nitakuonyoa kama si hivyo hutaingia," Nganga alisema

image
na KEZIA ACHIENG'

Dakia-udaku12 November 2024 - 09:20

Muhtasari


  • Mtume James Maina Ng’ang’a anawataka watu walio na nywele mtindo wa rasta kuzinyoa ndiposa wahudhurie kanisa lake.
  • Anawashauri wahubiri kufunza kuhusu ufalme wa mbinguni na sio pesa kwani pesa wataziacha humu duniani.


Mchungaji maarufu James Maina Ng’ang’a anawataka watu walio na nywele mtindo wa rasta kwanza kuzinyoa ili waweze kufika katika kanisa lake.

Katika video ya hivi majuzi aliyochapishwa kwenye TikTok, Ng’ang’a alisema kwamba wale ambao wana nywele mtindo wa rasta wanyoe na ikiwa yeyote ambaye ana rasta atamkaribia atamnyoa la sivyo hatoingia kwa kanisa lake na ikiwa ataingia itakuwa Jumapili moja pekee.

“We kama uko na rasta nyoa, utanyoa. Ukija mahali niko nitakuonyoa kama si hivyo hutaingia, utaingia Sunday moja hiyo ingine nitakunyoa,” alisema.

Mchungaji huyo pia alisisitiza kwamba ni wanawake ndio wameharibu kanisa lake kwani wanakuja na mavazi ambayo sio sawa kuvaliwa kanisani.

“Wamama nyinyi ndio mmeharibu kanisa hii na mnaweka rangi ni sawa, na kipaza sauti na huko umevaa suruali ile imevaliwa na koinange what is that eh? Huko unafanya vitu ambavyo ni vya kule nje lakini mdomo tu ndio Bwana asifiwe! Basi wewe ni muuwaji, we ni mwongo, we ni msengenyaji, we ni mwizi, we huna akili ya Mungu, akili zako ziko dunia, huna upendo, huna ushirika na roho wa Mungu, unaongea tu kila saa mambo ya serikali,”

Anawashauri wahubiri kufunza kuhusu ufalme wa mbinguni na sio pesa kwani pesa wataziacha humu duniani.

“Kuna Mungu juu mbinguni. Wale wameokoka, wale upcoming preachers preach about the kingdom of God not about the money. Pesa ni takataka tu utaziwacha tu. Dunia itakuhangaisha ikuhangaishe hutalala, ukipata milioni mbili unataka tano,”



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved