logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Shakib amsherehekea mwanawe wa kambo kwa ujumbe maalum

Shakib amemsherehekea mtoto wa pili wa mke wake Zari Hassan.

image
na Samuel Mainajournalist

Dakia-udaku02 January 2025 - 10:54

Muhtasari


  •  Mtoto huyo wa Zari na alisherehekea kutimiza miaka 17 na watu waliungana naye kuadhimisha siku hiyo maalum.
  • Raph ni mtoto wa pili wa Zari na aliyekuwa mume wake, marehemu Ivan Ssemwanga aliyefariki mwaka 2017


Raphael Ssemwanga, mtoto wa pili wa sosholaiti wa Uganda Zari Hassan hivi majuzi aliadhimisha siku yake ya kuzaliwa huku akiendelea kukua na kuwa mwanamume mkubwa.

 Mtoto huyo wa Zari na aliyekuwa mume wake marehemu Ivan Ssemwanga alisherehekea kutimiza miaka 17 na watu waliungana naye kuadhimisha siku hiyo maalum.

 Zari alitumia kurasa zake za mitandao ya kijamii kumsherehekea kijana huyo kwa kuchapisha picha zake nzuri. 

"Happy birthday to the realest @raphael.tlale," Zari aliandika.

 Mtu mwingine maalum ambaye alimsherehekea Raphael hadharani ni mume wa sasa wa Zari, Shakib Cham ambaye pia alikuwa na ujumbe mzuri kwa kijana huyo. 

"Heri ya siku ya kuzaliwa @raph, natumai kuwa leo ni mwanzo wa mwaka mzuri kwako," Shakib aliandika chini ya picha ya Raph.

Raph ni mtoto wa pili wa Zari na aliyekuwa mume wake, marehemu Ivan Ssemwanga aliyefariki mwaka 2017, miaka michache tu baada ya wawili hao kutengana.

 Kwa sasa ameolewa na Shakib Cham ambaye mara nyingi ameonyesha uhusiano wa karibu na watoto wake wote watano licha ya kutokuwa na mtoto pamoja.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved