logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Afisa wa zamani wa gereza ahukumiwa miezi 15 jela kwa kosa la kushiriki ngono na mfungwa

Wakati wa kusikilizwa kwa kesi dhidi yake Julai 2024, afisa huyo alikiri makosa ya utovu wa nidhamu katika ofisi ya umma mwezi.

image
na Brandon Asiema

Dakia-udaku07 January 2025 - 12:45

Muhtasari


  • Mshukiwa alipatikana na hatia ya kufanya ngono katika ofisi za umma na mfungwa.
  • Mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 30, alikamatwa akijaribu kutorokea Uhispania katika uwanja wa ndege wa Heathrow.


Aliyekuwa afisa wa zamani wa gereza moja nchini Uingereza amehukumiwa kifungo cha mwaka mmoja na miezi mitatu jela baada ya mahakama kumpata na hatia ya kushiriki ngono na mfungwa katika video iliyosambaa mitandaoni.

Afisa huyo wa zamani wa  gereza, alionekana kwenya video akishiriki mapenzi na mfungwa mmoja mnamo mwezi Juni mwaka uliopita wa 2024.

Katika uamuzi wake, mahakama imeeleza kuwa afisa huyo wa zamani amekuwa akifanya mapenzi mara kadhaa ikiwa ni tabia yake ya kujirudia.

Hata idara ya ujasusi ya polisi inaendeleza uchunguzi kuhusu wafungwa wawili waliotambulikwa kwenye kanda ya video iliyosambaa baada ya tukio hilo.

Mshukiwa huyo mwenye umri wa miaka 30, kwa mujibu wa shirika la habari la BBC limearififu kuwa alijaribu kutoroka ila maafisa wa polisi walimkamata katika uwanja wa ndege wa Heathrow katika jaribio la kutorokea Uhispania akiwa na baba wake.

Kufuatia kisa hicho kunadaiwa kwamba wafanyakazi wengi wa kike katika gereza alikokuwa anafanya kazi afisa huyo wa zamani wa gereza, kulikuwa na ripoti za ongezeko la visa vya ngono kutoka kwa wafungwa. Hii ni kwa mujibu wa ujumbe kwa njia wa maandishi kwa mahakama kutoka kwa gavana wa jimbo la Wandsworth Andrew Davy.

Gavana huyo alisema  wafanyakazi wengi wa kike katika gereza hilo wameripoti ongezeko la wafungwa kuwataka kimwili na sasa inachukuliwa kuwa mchezo wa haki.

Ushahidi uliowasilishwa kortini vile vile ulionyesha kuwa kulikuwa na tukio lingine mbali na lililosambaa la ngono baina ya afisa huyo na mfungwa huyo mmoja. Kanda za video kwenye camera za mwili kutoka kwa sare rasmi ya kazi ya afisa huyo zilionyesha hivyo.

Aidha wakati wa kusikilizwa kwa kesi dhidi yake mnamo mwezi Julai, afisa huyo alikiri makosa ya utovu wa nidhamu katika ofisi ya umma mwezi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved