logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Seneta Olekina ataka siasa ya Kenya kubadilishwa kuwa mchezo wa ndondi

Seneta huyo wa Narok amesema atakuwa mwamuzi katika mchuano wa kwanza baina ya Natembeya na 'Ichungua'

image
na Brandon Asiema

Dakia-udaku07 January 2025 - 11:26

Muhtasari


  • Kauli ya Olekina inajiri siku chache baada ya gavana Natembeya  na mbunge  Ichung’wah kufokeana hadharini katika mazishi ya mama wa spika Wetang'ula.


Seneta wa kaunti ya Narok Ledama Olekina ametania siasa ya Kenya kubadilishwa na kuwa mchezo wa ndondi akirejelea mizozano iliyoshuhudiwa katika mazishi ya mama wa spika wa bunge la kitaifa Moses Wetangula iliyofanyika wiki jana katika kaunti ya Bungoma.

Kwenye ukurasa wake wa X, seneta huyo wa aliyechaguliwa kwenye tiketi ya chama cha ODM aliashiria kuwa mwelekeo wa siasa humu nchini umegeuka na mbadala wake ni kufungua viwanja vya ndondi ili wanasiasa kumenyana.

“Mahali hii siasa imetufikisha itabidi sasa tufungue boxing rings! Wacha hii wanaume walimane…” Alisema Ledama Olekina kwenye ukurasa wake wa X awali Twitter.

Kwenye ujumbe wake huo, ujumbe wa  seneta Olekina umewalenga viongozi wawili ambapo ametaka gavana wa Trans Nzoia George Natembeya na mbunge wa Kikuyu Kimani Ichung’wah kuwa wa kwanza kwenye mechi ya ufunguzi. Olekina amesema kwamba yeye ndie atakuwa mwamuzi katika mchuano wa ndondi baina ya mbunge Ichung’wah na gavana Natembeya.

“Mechi ya kwanza Natembeya dhidi ya Ichungua. Mimi nitakuwa refa.” Alikiri Ledama Olekina.

Kauli ya Olekina inajiri siku chache baada ya gavana George Natembeya wa Trans Nzoia na mbunge wa Kikuyu Kimani Ichung’wah kufokeana hadharini kwa kutupiana cheche za maneno kuhusu mistakabali yao ya visa vya utekaji nyara wa vijana ambavyo vilishuhudiwa nchini ndani ya mwezi Disemba.

Kwa upande wake, gavana wa Trans Nzoia alimtaka rais William Ruto kuhakikisha visa vya utekaji nyara wa vijana unasitishwa kote nchini huku mbunge Kimani alimkashifu kuwa wakati kiongozi huyo(Natembeya) akiwa mtratibu wa bonfde la ufa, miili ya wakenya kutoka bonde la ufa ilipatikana kwenye mto Yala licha ya yeye kuwa kwenye idara ya polisi.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved