MWANAMUME mmoja anayefahamika kama mchungaji katika kanisa moja ameripotiwa kumuua bintiye mwenye umri wa miaka 16 anayeigua ugonjwa wa Down Synbdrome aimtuhumu kama mchawi.
Tukio hili la kushtua lilifichuliwa katika chapisho
lililosambaa kwenye jukwaa maarufu la mtandao wa kijamii, X, lililojulikana
kama Twitter.
Ndugu mdogo wa msichana huyo alisema baba yao alikusanya
familia na kutangaza kifo chake baada ya tukio hilo.
Ndugu mdogo alikumbuka kufungua mlango kumsaidia Dadake kutupa
kinyesi chake wakati baba yao alipoingilia kati, akisisitiza ashughulikie
mwenyewe. Alitii lakini akaanguka huku akirudi chumbani kwake.
Kijana alisema alimjulisha baba yao, ambaye aliingia
chumbani na kuwaambia wengine waondoke wakati yeye akimuhudumia bintiye. Baada
ya muda mrefu, Pasta aliwaita watoto wake ndani na kutangaza kufariki kwa binti
huyo.
Aliyeshiriki chapisho hilo aliyetambulika kwa jina la
@EduEle5 kupitia ukurasa wa X, alifichua kuwa polisi wamepewa taarifa na
mchungaji huyo kwa sasa yuko mbioni.
Mamlaka imeanzisha msako na pia inaomba umma usaidizi wa
kumpata na kumkamata.
Chapisho hilo lilisomeka, “Mtume Ubong Bassey Etim alimuua
bintiye mwenye umri wa miaka 16 huko Calabar baada ya kumshutumu kuwa mchawi
ambaye angeweza kubadilika na kuwa nyoka. Msichana huyo mchanga, ambaye alikuwa
na ugonjwa wa Down, aliuawa kikatili mnamo Februari 15, 2025, huko Calabar,
Jimbo la Cross River.”
“Mke wa mshukiwa aliyeachana naye alifichua kwamba pasta
alikuwa na historia ya unyanyasaji wa nyumbani, ambayo ilimlazimu kutoroka
nyumbani kwao. Pamoja na hayo, aliendelea kupigania usalama wa watoto wake.
Sasa anatoa wito kwa kusaidia kuhakikisha bintiye anapata haki.”
Tazama chapisho hilo hapa;