logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond asafirisha familia, wandani, washirika na Watanzania wengine sita hadi Qatar (+video)

Diamond alikiri kuwa na hamu kubwa ya kushuhudia Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza.

image
na Radio Jambo

Habari29 November 2022 - 03:43

Muhtasari


•Diamond alisafiri kwa ndege kutoka Tanzania hadi nchi hiyo ndogo ya Asia siku ya Jumatatu na aliandamana na kundi la wanafamilia,  marafiki na baadhi ya washirika wake.

•"Natamani kuona Brazil, Natamani nitazame Argentina nikamuone Messi. Pia natamani nimuone Mbappe," alisema.

Staa wa Bongo Diamond Platnumz yupo nchini Qatar kwa ajili ya kushuhudia moja kwa moja mechi za Kombe la Dunia.

Diamond alisafiri kwa ndege kutoka Tanzania hadi nchi hiyo ndogo ya Asia siku ya Jumatatu na aliandamana na kundi la wanafamilia,  marafiki na baadhi ya washirika wake.

Picha na video za safari hiyo zilichapishwa kwenye  ukurasa rasmi wa lebo ya WCB.

"Timu ya ushindi njiani kuelekea Qatar #Qatar2022 #FIFAWORLDCUP," taarifa iliyondakiwa chini ya video ya wasafiri walioandamana na Diamond ambayo ilichapishwa kwenye ukurasa wa Instagram wa WCB ilisoma.

Miongoni mwa walioandamana na bosi huyo wa WCB katika safari hiyo ni pamoja na Mama Dangote na mpenzi wake Uncle Shamte, Esma Platnumz, Mbosso, meneja Ricardo Momo, msemaji wa Yanga S.C Haji Manara, Baba Levo, Mwijaku pamoja na mlinzi rasmi wa Diamond Onesmo Amos.

Kabla ya kuabiri ndege, Diamond alisema kwamba alikuwa na hamu kubwa ya kusafiri hadi Qatar kushuhudia moja kwa moja michuano ya Kombe la Dunia kwa mara yake ya kwanza.

"Natamani kuona Brazil, Natamani nitazame Argentina nikamuone Messi. Pia natamani nimuone Mbappe," alisema.

Mwijaku ambaye hapo awali alikuwa chawa wa bosi wa Konde Music Worldwide Harmonize kabla ya kumtema na kuungana na Diamond alionekena kuifurahia sana safari hiyo kwa kuwa walikaa sehemu ya VIP.

"Huduma za VVIP, matajiri tumeingia DOHA kwa hisani ya Wasafibet," aliandika chini ya video iliyoonyesha akiwa ndani ya ndege.

Pamoja nao katika ndege hiyo walikuwepo Watanzania wengine sita waliofadhiliwa na Wasafi Bet yake Diamond Platnumz.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved