logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Hakikisha umejijenga kwanza kabla ya kujitosa kwenye ndoa " Carol Muthoni awashauri wanadada

Muthoni pia alifichua kuwa wanaume wengi wamekuwa wakimmezea mate.

image
na Radio Jambo

Makala22 March 2022 - 19:47

Muhtasari


•Muthoni aliwashauri wanawake kuhakikisha kuwa wako sawa kifedha, kiakili na kihisia kabla ya kujitosa kwenye ndoa.

•Muthoni pia alifichua kuwa wanaume wengi wamekuwa wakimmezea mate. Hata hivyo amewasihi watulie kidogo kwanza. 

Carrol Sonnie katika studio za Radio Jambo

Mwigizaji Caroline Muthoni almaarufu Carrol Sonnie amewashauri wanadada kutokubali shinikizo la jamii kuhusu umri mwafaka wa kuolewa.

Akizungumza kwenye ukurasa wake wa Instagram, Muthoni alisema kwamba umri sio jambo muhimu zaidi kuzingatia katika mpango wa ndoa.

Mpenzi huyo wa zamani wa mchekeshaji Mulamwah aliwashauri wanawake kuhakikisha kuwa wako sawa kifedha, kiakili na kihisia kabla ya kuzamia kwenye ndoa.

"Olewa ukiwa tayari. Hakikisha uko katika nafasi ambayo unaweza kujisimamia, usitegemee mpenzi wako. Wanawake, kabla ya kuingia kwenye ndoa tafadhali hakikisha umejijenga kwanza. Kuwa sawa kiakili, kifedha na kihisia," Muthoni alisema.

Mama huyo wa binti mmoja aliwahimiza wanawake kukimbiza ndoto zao kwanza huku akiwahakikishia kwamba mengine yatajileta baadae.

"Tafuta pesa ujijenge kwanza. Mengine yatajileta," Alisema.

Muthoni pia alifichua kuwa wanaume wengi wamekuwa wakimmezea mate. Hata hivyo amewasihi watulie kidogo kwanza. 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved