logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize aonyesha mapenzi makubwa kwa Eve Mungai, mpenziwe ajibu "Hii imeenda!"

"Hii imeenda πŸ˜‚πŸ˜‚ Harusi ni lini Mmakonde," Trevor alisema.

image
na Radio Jambo

Dakia-udaku06 February 2023 - 07:55

Muhtasari


β€’Baada ya kuwasili, Konde Boy  alishiriki mahojiano na mtangazaji huyo ambapo alizungumzia masuala mbalimbali.

β€’Bosi huyo wa Kondegang pia aliendelea kuonyesha upendo kwa Eve chini ya video yake ambayo alichapisha kwenye Instagram.

Staa wa Bongo Rajab Abdul Kahali almaarufu Harmonize ameonyesha upendo kwa mhoji maarufu wa Kenya, Eve Mungai.

Wawili hao walikutana siku ya Jumamosi katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Jomo Kenyatta, jijini Nairobi wakati alipowasili kwa ajili ya shoo yake kubwa mjini Embu ambayo ilifanyika usiku wa Jumamosi.

Baada ya kuwasili, Konde Boy  alishiriki mahojiano na mtangazaji huyo ambapo alizungumzia masuala mbalimbali.

"Niko hapa na mrembo Eve na tunaenda Embu usiku wa leo. Itakuwa wazimu. Ninaita kila mtu kujitokeza. Usikose hii," mwimbaji huyo alisema baada ya mahojiano.

Baada ya mahojiano, Eve aliungana na staa huyo wa Bongo kwa tamasha lake la usiku katika kilabu moja mjini Embu.

Mtangazaji huyo alipojitokeza kwenye jukwaa, Harmonize alishindwa kujizuia na kukiri jinsi alivyoonekana mzuri.

"Unaonekana mzuri sana usiku wa leo," alisema Harmonize.

Bosi huyo wa Kondegang pia aliendelea kuonyesha upendo kwa Eve chini ya video yake ambayo alichapisha kwenye Instagram.

"MALKIAπŸ‘Έβ€οΈ" Harmonize aliandika kwenye video ya Eve  akitembea kwa madaha.

Eve aliambatanisha video hiyo kwa wimbo wa Harmonize na Ibraah "One night stand"

Staa huyo wa Bongo pia alichora emoji za upendo chini ya video nyingine ya Eve ambayo alichapisha Jumapili. Eve kwa upande wake pia alijibu kwa emoji ya moyo ambayo kwa kawaida huashiria upendo.

Wanamitandao wamekuwa na maoni tofauti kuhusu shughuli za hivi majuzi za wawili hao huku wengine wakienda hadi kukisia kuwa kuna mahapa yanayojengwa kati yao.

Mpenzi wa Eve, Director Trevor ni miongoni mwa ambao wameweza kutoa maoni kuhusu matendo ya wawili hao.

"Hii imeenda πŸ˜‚πŸ˜‚ Harusi ni lini Mmakonde," alisema.

Wanamitandao wengine wengi walikubaliana na maoni ya Trevor huku makumi pia wakitoa maoni, "Hii imeenda"

Katika jibu lake, Eve alisema "Mtulie bana"


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logoΒ© Radio Jambo 2024. All rights reserved