logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Nina haki ya kufanya chochote!" Nandy afunguka kuhusu kusoma meseji za mumewe Billnass

Mapema mwaka huu, rapa Billnass alimvisha Nandy pete ya uchumba baada yake kukubali ndoa naye.

image
na Radio Jambo

Burudani05 April 2022 - 20:20

Muhtasari


•Nandy alisema mpenzi wake yupo huru kuchukua simu yake na vilevile mumewe hajawahi kumzuia yeye kuchukua simu yake.

•Mapema mwaka huu, rapa Billnass alimvisha Nandy pete ya uchumba baada yake kukubali ndoa naye.

Billnass na Nandy

Mwanamuziki wa Bongo Faustina Mfinanga almaarufu kama Nandy amefichua kwamba yeye na mpenzi wake Bill Nass hubadilishana simu wakati wowote.

Akihutubia waandishi wa habari katika hafla ya kuzindua Funguka Campaign, Nandy alisema mpenzi wake yupo huru kuchukua simu yake na vilevile mumewe hajawahi kumzuia yeye kuchukua simu yake.

"Ni kama tunatumia simu zetu pamoja. Simu yake naweza nikachukua muda wowote, simu yangu anaweza akachukua muda wowote. Sidhani kama atakuwa anachukua aende kusoma jumbe  moja kwa moja. Ana haki ya kufanya chochote, pia mimi nina haki ya kufanya chochote kwenye simu yake," Nandy alisema.

Malkia huyo wa muziki alikiri kwamba huwa anapitia jumbe zilizo kwenye simu ya mumewe. Hata hivyo alisisitiza kwamba hana shaka naye na anamwamini sana.

"Siwangi rasmi eti nataka kusoma kwa sababu nina shaka naye, hapana. Namwamini!" Alisema.

Mapema mwaka huu, rapa Billnass alimvisha Nandy pete ya uchumba baada yake kukubali ndoa naye. 

Billnass aliposa kwa mpenzi huyo wake mwezi Februari na kwa mara ya pili Nandy akakubali kufunga pingu za maisha naye.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved