logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Sikuhitaji kueleza chochote" Mimi Mars asema kuhusiana na Marioo kuumia baada yake kuogelea na Diamond

Mars ameshikilia msimamo kuwa uhusiano wake na Marioo ni wa kirafiki tu.

image
na Radio Jambo

Habari09 June 2022 - 07:07

Muhtasari


•Malkia huyo  ambaye ni dada wa Vanessa Mdee ameshikilia msimamo kuwa uhusiano wake na Marioo ni wa kirafiki tu.

•Mars pia alifichua kuwa hakuwahi kujua kuwa tukio la yeye kuonekana kwenye bwawa la kuogelea na Diamond lilimuumiza Marioo

Marioo na mpenzi wake Mimi Mars

Mwanamuziki na mtangazaji Mimi Mars amesisitiza kuwa hakuna uhusiano wa kimapenzi kati yake na Marioo.

Malkia huyo  ambaye ni dada wa Vanessa Mdee ameshikilia msimamo kuwa uhusiano wake na Marioo ni wa kirafiki tu.

"Mimi na Marioo hatupo kwenye mahusiano. Tuna mahusiano ya kirafiki ambayo ni mazuri. Nahisi hicho dicho kinasababisha watu kusema tupo kwenye mahusiano," Mars alisema katika mahojiano na Wasafi Media.

Mars hata hivyo hakutupilia mbali uwezekano wa wao kujitosa kwenye mahusiano katika siku za usoni.

"Wakati mwingine urafiki huko mbeleni mambo yakikorea yanaweza kuwa mazuri lakini ikitokea mtajua. Sisi wenyewe ndio tutasema lakini kwa sasa hamna kitu," Mars alisema.

Hata hivyo aliweka wazi kuwa tayari yupo kwenye mahusiano mengine na mwanaume ambaye sio maarufu. Alifichua kuwa mpenzi wake ni raia wa Tanzania.

Alieleza kuwa alikuja kufahamu kuhusu hayo hivi majuzi wakati Marioo alifunguka kupitia Instastori zake.

"Sidhani kama nilihitaji kumweleza chochote. Sikujua chochote muda huo eti angeumia. Mimi mwenyewe nilikuja kujua juzi alipoweka kwenye Instastori zake. Hakuwahi kuniambia," Alisema.

Hata hivyo aliweka wazi kuwa hakukerwa na hatua ya Marioo kufunguka kuhusu hisia zake kufuatia tukio hilo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved