logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Trio Mio afunguka kuhusu kuchumbiana na mwanamke mzee

"Inategemea uhusiano. Lakini sitawahi kuchumbiana na mwanamke mzee," alisema.

image
na

Makala20 December 2022 - 03:55

Muhtasari


•Katika mahojiano na Mungai Eve, Trio Mio alibainisha kuwa anawaheshimu wanawake walio juu yake kiumri.

•Rapa huyo mdogo alimmwagia sifa mpenzi wake.

Mwimbaji mdogo wa muziki wa kisasa Trio Mio anasema babake alimshauri asiwahi kuchumbiana na mwanamke mzee.

Katika mahojiano na Mungai Eve, Trio Mio alibainisha kuwa anawaheshimu wanawake walio juu yake kiumri.

"Inategemea uhusiano. Lakini sitawahi kuchumbiana na mwanamke mzee. Ni ukweli," alisema.

"Tukiwa umri sawa zogo inaweza zua, mnaeza katsiana vibaya sana na mimi staki, so nitachumbiana na mtu ambaye ni mdogo kuliko mimi."

Mwaka wa 2021, mama yake, Irma Sakwa, alisema kuwa alikutana na mpenzi wa Trio na kuidhinisha.

"Nilifurahi angalau ameleta msichana na nimekutana naye. Ni vizuri. Ni bora kuliko kuweka uhusiano kuwa siri."

Rapa huyo mdogo alimmwagia sifa mpenzi wake.

"Yeye ni mrembo, ananifurahisha, ni msikivu," alisema.

"Nataka kufikia malengo yangu kwani yeye anafanikisha yake tukiwa bado pamoja."


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved