logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Yule kakosea, sikupendezwa!" Babake Diamond amkosoa kwa kutobolewa pua

Mzee Abdul alisema Diamond anapaswa kuangazia mambo mengine ya kujirembesha.

image
na Radio Jambo

Habari01 November 2022 - 12:41

Muhtasari


•"Yule kakosea kweli. Kutokana na maadili yetu sisi, watoto wa kiume hawapaswi kufanya vitu kama hivyo," alisema.

•Mzee Abdul alisema ikiwa Diamond ataendelea na tabia zile huenda akapoteza mashabiki.

Mzee Abdul Juma Isack amekosoa kitendo cha mwanawe Diamond Platnumz kutobolewa pua.

Wiki chache zilizopita, Diamond alichapisha video iliyoonyesha akitobolewa upande moja wa pua lake na kuwekwa herini. Hatua hiyo ilizua hisia mseto huku baadhi wakifurahishwa nayo na wengine wakimkosoa.

Mzee Abdul ambaye anaaminika kuwa baba mzazi wa staa huyo wa Bongo ameweka wazi kuwa jambo hilo halikumfurahisha.

"Yule kakosea kweli. Kutokana na maadili yetu sisi, watoto wa kiume hawapaswi kufanya vitu kama hivyo," alisema katika mahojiano na Mbengo TV.

Abdul alidai kuwa huenda mwimbaji huyo alichukua hatua hiyo kutokana na ustaa wake, utajiri, uwezo na kiburi.

Alisema Diamond anapaswa kuangazia mambo mengine ya kujirembesha bali na yanayokiuka maadili ya Kitanzania.

"Hayo sio maadili ya Kitanzania. Ni maadili ya mbali ya Kinyamwezi. Kusema kweli sikupendezwa na lile suala, aangalie kama kuna vitu vingine vya kugeza,"

Aidha alibainisha kuwa wasanii wengine wakubwa kama vile Ali kiba hawajaiga tabia kama za kujitoboa pua.

"Zamani tulikuwa na mitindo ya kujichorachora mwilini lakini sasa hivi tunajutia" alisema.

Amemshauri mwanamuziki huyo kutema mienendo isiyo ya kimaadili. Alisema ikiwa Diamond ataendelea na tabia zile huenda akapoteza mashabiki.

Abdul pia aliwaomba watu wa karibu na mwawe kumshauri kuhusu maadili mema.

Mzee Abdul alikiri kuwa muda mrefu umepita tangu alipomuona mwanawe kwa mara ya mwisho. Hata hivyo alieleza matumaini yake kuwa siku moja bosi huyo wa WCB atachukua hatua ya kumtembelea.

"Labda ana pilkapilka nyingi za kikazi. Labda anakosa kutulia akitafuta maisha. Ipo siku, kama ilivyotokea akanipa salamu, ipo siku atakuja kunipa salamu," alisema.

Mzee Abdul anaaminika kuwa baba mzazI wa Diamond. Hata hivyo, takriban miaka miwili iliyopita, familia ya Diamond ikiongozwa na mama yake Mama Dangote ilionekana kumkana na kujitenga naye.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved