logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Je, Bahati ameacha injili? Tazama kibao chake kipya

Kwenye kibao hicho, Bahati amesikika akiwadhalilisha wasanii wengine kama Sauti Saul, Ringtone, Khaligraph na Octopizzo.. Khaligraph amjibu

image
na Radio Jambo

Yanayojiri08 June 2021 - 08:48

Muhtasari


•"Alafu naskia Bahati ameanza bangi na sigara ameanza kurap matusi, punguza iyo bangi baba wacha kiherehere" Khaligraph alimjibu Bahati.

•Kwenye video hiyo, Bahati pia anaonekana kwenye klabu akivuta sigara kubwa

Bahati

Mwanamuziki wa nyimbo za injili  na mapenzi Kelvin Kioko ameachilia kibao kipya kwa jina 'Fikra za Bahati' kwenye mtandao wa Youtube.

Kwenye kibao hicho, Bahati amesikika akiwadhalilisha wasanii wengine kama Sauti Saul, Khaligraph na Octopizzo.

Picha za video hiyo zilizokuwa zimeonyeshwa kabla ya video kuachiliwa na ambazo zilionyesha Bahati akivuta sigara kubwa zilikuwa zimeibua hisia mbalimbali miongoni mwa Wakenya huku ikisemekana kuwa huenda msanii huyo ameiaga injili.

Ringtone ni mmoja wa wasanii waliomkahifu Bahati huku akisema kuwa Bahati alikuwa ameacha injili na kuingilia utumizi wa madawa ya kulevya.

 

Khaligraph ambaye kwa sasa ako katika ziara nchini Marekani amemjibu Bahati huku akimwambia awache bangi na apunguze Kiherehere.

"Alafu naskia Bahati ameanza bangi na sigara ameanza kurap matusi, punguza iyo bangi baba wacha kiherehere" Khaligraph alimjibu Bahati.

Bahati amesema kuwa kibao hicho ni cha kuwatayarisha mashabiki wake kwa albamu yake 'Love like this' ambayo ataachilia hivi karibuni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved