logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Limousine, Karamu; Sonko atoa zawadi nono kwa Omanyala baada ya kushinda dhahabu

• Omanyala aliishindia Kenya dhahabu ya kwanza kabisa katika mbio za mita 100 kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola. •Sonko pia alimhakikishia Omanyala kuhusu upendo mkubwa wa Wakenya kwake kwa kuleta utukufu nyumbani na kutufanya tujivunie.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri04 August 2022 - 09:34

Muhtasari


• Omanyala aliishindia Kenya dhahabu ya kwanza kabisa katika mbio za mita 100 kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola.

•Sonko pia alimhakikishia Omanyala kuhusu upendo mkubwa wa Wakenya kwake kwa kuleta utukufu nyumbani na kutufanya tujivunie.

Aliyekuwa gavana wa Nairobi Mike Sonko amedokeza kuhusu mpango wake wa kumzawadia mwanariadha Ferdinand Omanyala na gari aina ya Limousine baada ya kutwaa dhahabu kwenye mashindano ya Jumuiya ya madola yanayoendelea jijini Birmingham, Uingereza.

Jumatano usiku Omanyala aliishindia Kenya dhahabu ya kwanza kabisa katika mbio za mita 100 kwenye mashindano ya Jumuiya ya Madola  alipoibuka  wa kwanza baada ya kukimbia kwa sekunde 10.02.

Sonko ni mmoja wa waliompongeza Omanyala huku akiiomba serikali ya Kenya kumruhusu amuandalie bingwa huyo wa Afrika katika mbio za mita 100 mapokezi mazuri na sherehe kubwa  atakapokuwa akirejea nchini.

"Mlipokuwa mmelala mnaota Mkenya mmoja ambaye ni  mwanaume mwenye mbio kubwa zaidi Afrika nzima Ferdinand Omanyala ameshindia nchi ya Kenya dhahabu kwenye Commonwealth Games, akiandikisha sekunde 10.02. Pongezi sana na serikali ikikubali nitakupangia sherehe kubwa ya kukuaki na limousines 15 zikupokee na nikufanyie shereye ya 10 days na nikupee limo moja bure iwe yako," Sonko alisema kupitia ukurasa wake wa Facebook.

Mwanasiasa huyo pia alimhakikishia Omanyala kuhusu upendo mkubwa wa Wakenya kwake kwa kuleta utukufu nyumbani na kutufanya tujivunie.

Omanyala akisherehekea ushindi wake baada ya kutwaa dhahabu aliwashukuru wote waliounga mkono azma yake ya kupata ubingwa.

Isaya 55.5 , Kwa utukufu wa Bwana wetu Yesu Kristo. Asanteni sana kwa uungwaji mkono na motisha," Omanyala alisema kupitia ukurasa wake wa Twitter.

Aliongeza "BINGWA WA AFRIKA sasa ndiye BINGWA WA JUMUIYA YA MADOLA!"

Maelfu ya Wakenya wakiwemo viongozi na watu maarufu  wameendelea kumpongeza bingwa huyo wa mbio za mita 100  kupitia mitandao ya kijamii.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved