logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mcheshi Erick Omondi adinda kulipa deni baada ya kula uroda na kidosho, Nairobi.

Mcheshi Erick Omondi amekashifiwa kwa kula uroda na msichana katika hoteli moja jijini Nairobi halafu akakosa kutimiza ahadi ya kulipa binti huyo shilingi elfu ishirii na tano.

image
na

Makala02 February 2022 - 08:23

Muhtasari


• Mcheshi Erick Omondi amekashifiwa kwa kula uroda na msichana katika hoteli moja jijini Nairobi halafu akakosa kutimiza ahadi ya kulipa binti huyo shilingi elfu ishirii na tano.

• Hata hivyo ni zaidi ya mwaka mmoja sasa na Erick Omondi hajaweza kutimiza ahadi yake , jambo lililomlazimu manzi wa TRM kuchapisha ujumbe katika mtandao wa Instagram kumsuta Erick Omondi kwa kuwa mdanganyifu na kukosa kuchukua simu zake alipompigia.

Eric Omondi

Mcheshi Erick Omondi amekashifiwa kwa kula uroda na msichana katika hoteli moja jijini Nairobi halafu akakosa kutimiza ahadi ya kulipa binti huyo shilingi elfu ishirii na tano.

Akizungumza na chombo kimoja cha habari, msichana huyu almaarufu manzi wa TRM alisema kwamba alikutana na Omondi katika sehemu moja ya kujistarehesha halafu baadaye mcheshi huyo akamuomba wakatulie katika hoteli ya kifahari mjini ili kujuana zaidi.

Manzi wa TRM anasema kwamba siku hiyo Erick Omondi alisema alikosa kwenda nyumbani kwa kile alichokitaja kuwa kulikuwa na aila yake pale na hivyo hawangepata muda mzuri wa kutangamana na kidosho huyo.

Aidha, binti huyo alikiri kwamba alimwelezea Omondi kwamba ana changamoto ya kulipa ada ya sehemu alimokuwa akiishi, huku rais huyo wa ucheshi akiahidi kugharamikia ada hiyo ambayo ilikuwa takribani shilingi elfu ishirini na tano.

Hata hivyo ni zaidi ya mwaka mmoja sasa na Erick Omondi hajaweza kutimiza ahadi yake , jambo lililomlazimu manzi wa TRM kuchapisha ujumbe katika mtandao wa Instagram kumsuta Erick Omondi kwa kuwa mdanganyifu na kukosa kuchukua simu zake alipompigia.

Kwa sasa inasubiriwa kuona iwapo Omondi atafanya kweli na kulipa deni.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved