logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Msidanganywe!Kiki tunazitengeneza sisi - Willy Paul

Pozze amesema wanatengeneza kiki wenyewe, huku akiwaomba msamaha mashabiki.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri10 February 2022 - 09:18

Muhtasari


• Msanii Willy Paul amekiri kwamba baadhi ya kiki zinapangwa na wasanii wenyewe ili kusukuma miziki yao kufikia watu wengi.

• Pozze amewaomba radhi mashabiki wake kwa wakati wote ambao amefanya kiki ili kusukuma ngoma zake na kuwahakikishia kwamba atakuwa anatia bidii zaidi kutoa ngoma nzuri zinazojiuza bila kiki.

Willy Paul

Msanii Willy Paul amekiri kwamba baadhi ya kiki zinapangwa na wasanii wenyewe ili kusukuma miziki yao kufikia watu wengi.

Kupitia ujumbe alioachia katika ukurasa wake wa Instagram, Pozze amewaomba radhi mashabiki wake kwa wakati wote ambao amefanya kiki ili kusukuma ngoma zake na kuwahakikishia kwamba atakuwa anatia bidii zaidi kutoa ngoma nzuri zinazojiuza bila kiki.

“Samahani mashabiki wangu, mwaka huu ni pure music,” aliandika Willy Paul.

 Kwa upande wa mashabiki, wameonyesha kukerwa na hali hiyo huku wakisema kwamba wasanii wamekuwa wakiwachukulia poa kwa muda mrefu huku wakwarai kujikita katika kufanya muziki mzuri bila kiki.

Aidha kuna wale walionekana kumkashifu Willy Paul wakisema kwamba manii huyo hawezi kufanya vizuri katika burudani la humu nchini bila kiki.

Swala ambalo kwalo wengi wanazidi kujikuna vichwa ni iwapo ile kesi ya Willy Paul kujaribu kumnajisi Diana Marua ilikuwa kweli ama miongoni mwa kiki zake za kawaida.

Kwa sasa mashabiki watalazimika kusubiri kuona iwapo msanii huyo atatimiza ahadi aliyotoa kwao kadri siku zinavyosonga.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved