logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Fanyeni kazi wasanii, msipende kiki - Octopizzo

Octopizzo ameonyesha kukasirishwa na wasanii ambao wanafanya kiki kwenye muziki.

image
na

Yanayojiri16 February 2022 - 10:31

Muhtasari


• Msanii Octopizzo ameonyesha kukasirishwa kwake kwa wanamuziki na wasanii wote ambao wanajihusisha katika masuala ya kutengeneza kiki.

• Octopizzo ni moja kati ya rapa ambao hawajihusishi na vurugu nyingi kwenye gemu la burudani, jambo ambalo limemfanya kudumu kwenye muziki kwa muda mrefu.

Octopizzo

Rapa matata Octopizzo ameonyesha kukasirishwa kwake kwa wanamuziki na wasanii wote ambao wanajihusisha katika masuala ya kutengeneza kiki.

Kupitia ujumbe aliochapisha katika ukurasa wake wa Instagram, Pizzo amewauliza wasanii iwapo wanafanya kiki ili kujikuza kikazi au kutafuta umaarufu.

“Mnaotafuta kiki, wasanii na wanamuziki, je mnafanya hivo kukuza vipaji vyenu ama kupata umaarufu?” Aliuliza Octopizzo.

Katika siku za hivi karibuni wanamuziki wengine wameonekana kufanya kiki ili kusukuma kazi zao, jambo ambalo msanii Octopizzo hajalipokea kwa furaha.

Kulingana naye, angependelea wasanii kutia bidii katika kutoa nyimbo nzuri ambazo zitapokelewa na mashabiki bila ugumu wowote utakaolazimu wao kutoa kiki.

Octopizzo ni moja kati ya rapa ambao hawajihusishi na vurugu nyingi kwenye gemu la burudani, jambo ambalo limemfanya kudumu kwenye muziki kwa muda mrefu.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved