logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mwanahabari Sean Cardovillis aomba msaada wa matibabu

Sean Cardovillis amewaomba wahisani kumpa msaada wa kulipia ada ya matibabu.

image
na Radio Jambo

Habari17 February 2022 - 08:19

Muhtasari


• Aliyekuwa mwanahabari wa runinga ya NTV Sean Cardovilis amahitaji msaada wa wahisani wema ili kulipia ada ya matibabu ambayo imekwea mara dufu.

Aliyekuwa mwanahabari wa runinga ya NTV Sean Cardovilis amahitaji msaada wa wahisani wema ili kulipia ada ya matibabu ambayo imekwea mara dufu.

Cardovilis ambaye alikuwa mwanahabari wa michezo katika runinga hiyo aliachishwa kazi baada ya janga la Corona kubisha hodi nchini, jambo lililosababishia mashirika mengi na makampuni kupunguza wafanyakazi wake.

Cardovilis ambaye ana uzoefu wa kazi kwa Zaidi ya miaka 20 alifutwa kazi Pamoja na wenzake kama vile Ken Mijungu na Debarl Inea baada ya janga la Corona kulemaza shughuli nyingi za shirika la Nation.

Katika bango ambalo limesambazwa mitandaoni ni wanahabari na watangazaji mbali mbali, Cardovilis anahitaji msaada ili kulipia gharama ya matibabu ambayo imepiku uwezo wake na anahitaji kusaidia.

“Sean amelazwa sasa kwa muda. Maumivu ya kifua aliyokuwa akiyapata kwa muda yaligeuka na kuwa nimonia na pafu lake moja likafeli. Pia alikuwa na matatizo ya moyo wake. Anazidi kupata matibabu ya kitaalamu na anaendelea vizuri lakini anahitaji ufuatiliaji na uangalizi wa karibu Zaidi,” maandiko katika bango hilo yalisoma.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved