logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nimeokoka, huu mwaka nataka kubatizwa! - Kartelo

Mchekeshaji Kartelo amesema ameokoka na huu mwaka anataka kubatizwa

image
na Radio Jambo

Makala23 February 2022 - 08:13

Muhtasari


• Mchekeshaji na msanii Kartelo ameweka wazi malengo yake ya mwaka huu na miongoni mwao ni kubatizwa kwa sababu alishaokoka.

Kartelo

Mchekeshaji na msanii Kartelo ameweka wazi malengo yake ya mwaka huu na miongoni mwao ni kubatizwa kwa sababu alishaokoka.

Akizungumza na Mungai Eve, Kartelo alisema kwamba ameokoka na anatarajia kubatizwa mwaka huu kwani Yesu ni mwokozi wake.

“Mi hukuwa mtu wa church tangu kitambo. Saa hii nimeokolewa. Yesu ni Mwokozi. Huu mwaka, nataka kuwa baptized,” alisema Kartelo.

Mchekeshaji huyo ambaye alivuma sana kati yam waka 2019 na 2020 alipoulizwa ukimya wake kutoka kwenye mitandao ya kijamii alisema kwamba ni uamuzi wa kibafsi na alifanya hivo ili kujipatia muda Zaidi wa kujitathmini.

"Nafocus na vitu personal kama familia, mamorio, spiritual growth na project zangu personal. Kutumia mokoro pesa sio enough," alisema Kartelo.

Kartelo ambaye kwa muda mrefu ametajwa kuwa na ugomvi wa chini kwa chini na mchekeshaji mwenza Chipukeezy pia alifichua kwamba amemsamehe na hana beef na yeye na kusema kwamba yuko tayari kufanya kazi pamoja na Chipukeezy kama itatokea na aone inamfaidi.

“Mimi namrespect sana kwa sababu Chipukeezy amenivusha daraja mingi sana na tumeokoleana sana. Tumejengana sana na amenisaidia sana. Out of hiyo respect, siwezi kuwa na chuki na yeye. Mimi siwezi kosa ku work na yeye na that’s if mtu ako willing tutafanya kazi,” alisema Kartelo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved