logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Umepigana vita kwa ajili yangu,'Grace Ekirapa amsherehekea dada yake

Grace anatarajia mwanawe wake wa kwanza na mumewe muigizaji Pascal Tokodi.

image
na Radio Jambo

Habari03 March 2022 - 10:19

Muhtasari


  • Grace Ekirapa ni miongoni mwa watangazaji wanaosherehekewa sana nchini na wanamitandao
grace ekirapa

Grace Ekirapa ni miongoni mwa watangazaji wanaosherehekewa sana nchini na wanamitandao.

Grace anatarajia mwanawe wake wa kwanza na mumewe muigizaji Pascal Tokodi.

Kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram alisherehekea siku ya kuzaliwa ya dada yake kwa ujumbe maalum.

Grace alimlimbikizia sifa dada yake huku akisema kwamba amepigana vita kwa ajili yake, na kumtetea mahali hangeweza kujitetea.

"Kwa mzaliwa wetu wa mwisho ambaye anakataa kutenda kama mmoja. Wewe ni gem katika maisha yangu. Umenipigania vita, umenitetea mahali nisingeweza kufanya mwenyewe, umenishika mkono na kunisaidia kuinuka nilipodhani nitazama na bado unafanikiwa kuwa peke yangu unaniudhi,

@juliet.ekirapa nakupenda sana na naomba Mungu atulinde milele na kama sivyo basi atuvushe pamoja maana siwezi kuona maisha yangu bila wewe. Ninasherehekea mwanamke mwenye nguvu ambaye umekuwa.

Jinsi unavyorudi nyuma kutoka kwa misimu migumu ni kitu ninachovutiwa nawe na ninakuombea mtoto wangu akope baadhi ya sifa zako ili niwe na ukumbusho wako kila wakati nyumban,Happy Birthday Dada yangu Mdogo. Nakupenda."

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved