logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nadia Mukami na Arrow Bwoy wazindua wakfu kwa heshima ya mtoto waliyepoteza

Nadia alisema kwamba alipata wazo hilo baada yaujauzito wake wa kwanza kuharibika mwaka jana.

image
na Radio Jambo

Habari09 March 2022 - 04:32

Muhtasari


•Nadia alisema Lola & Safari Foundation italenga wasichana wadogo na kina mama ambao hukabiliwa na changamoto katika kipindi cha ujauzito.

•Mwanamuziki huyo alisema kwamba alipata wazo hilo baada yaujauzito wake wa kwanza kuharibika mwaka jana.

Nadia Mukami na Arrow Buoy katika hafla ya uzinduzi wa Lola and Safari Foundation

Wanandoa mashuhuri Nadia Mukami na Arrow Bwoy wamezindua wakfu mpya kwa jina Lola & Safari Foundation.

Akihutubia wanahabari katika hafla ya uzinduzi iliyofanyika Jumanne, Nadia alisema Lola & Safari Foundation italenga wasichana wadogo na kina mama ambao hukabiliwa na changamoto katika kipindi cha ujauzito.

Malkia huyo wa muziki alisema walipatia wakfu huo jina 'Lola & Safari' kwa heshima ya mtoto wao ambaye alikufa tumboni kabla ya kuzaliwa.

"Lola & Safari ni jina ambalo tulikusudia kupatia mtoto wetu lakini hatukufika hapo. Sihitaji kulizungumzia kwa sasa. Ni wakfu muhimu sana kwetu. Ni kitu kizuri hapa. Katika Lola & Safari Foundation tutasaidia, kuelimisha na kushauri wasichana na kina mama wadogo," Nadia alisema.

Mwanamuziki huyo alisema kwamba alipata wazo hilo baada yaujauzito wake wa kwanza kuharibika mwaka jana. 

Alisema matatizo ambayo alishuhudia wakati wa ujauzito wake yalimsukuma kutafuta washirika ili kuanzisha mradi huo.

"Lola & Safari ya Nadia Mukami na Arrow Bwoy ni Wakfu unaolenga wasichana na akina mama wadogo ambao wanapitia changamoto za ujauzito, kuzaa, unyogovu baada ya kuzaa na wale ambao hawawezi kumudu huduma za afya ya uzazi na pia kuja na mpango sahihi wa kifedha. Lola na Safari Foundation pia inaangazia wasichana matineja ambao wameacha shule kwa sababu ya mimba za utotonina inatoa uhamasishaji kwa wasichana wachanga juu ya ujauzito," Nadia alisema.

Wanandoa hao walisema watakuwa wanafanya tamasha za hisani, kutembelea mitaa ya mabanda na kufanya michango katika juhudi za kufanikisha ndoto yao ya kusaidia wanawake katika safari zao za ujauzito.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved