logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Babalevo asema mwaka huu Diamond atawazima wasanii wengi

Babalevo ameendeleza kampeni ya kumshabikia Simba akisema mwaka huu atatasua sana.

image
na Radio Jambo

Habari11 March 2022 - 08:09

Muhtasari


• Msanii kutoka Tanzania, Babalevo amesema kwamba mwaka huu Diamond Platinumz anakwenda kufanya mambo mengi makubwa na kuwatoa kijasho wasanii wenzake katika gemu la burudani.

• “Diamond alisema mwaka huu anakwenda kufanana na hela zake, watu watachoka sana na kazi,” Babalevo alisema.

Msanii kutoka Tanzania, Babalevo amesema kwamba mwaka huu Diamond Platinumz anakwenda kufanya mambo mengi makubwa na kuwatoa kijasho wasanii wenzake katika gemu la burudani.

 Akizungumza Alhamisi katika uzinduzi wa EP ya Diamond Platinumz, Babalevo alisema kwamba kutokana na wingi wa hela alizonazo Simba, atakuwa anaachia kazi kali ambazo zitabaki kwenye kumbukumbu.

“Diamond alisema mwaka huu anakwenda kufanana na hela zake, watu watachoka sana na kazi,” Babalevo alisema.

Babalevo alisisitiza kwamba Simba ndiye msanii wa kipekee ambaye anaweza kupeleka muziki wa bongo katika viwango vya kimataifa.

Kwa upande wake alisema muda rasmi hujawadia kwake kuachia EP akisema anataka kupata mashabiki wa kutosha.

Mwanamuziki huyo ambaye pia ni mtangazaji katika Wasafi fm, ni moja kati ya watu ambao ni ‘chawa’ wake Diamond Platinumz.

Kwa sasa inasubiriwa kuona EP hiyo itafanya vipi katika gemu la Bongo na Afrika Mashariki.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved