logo

NOW ON AIR

Listen in Live

EP ya Diamond ilichaguliwa kutoka kwa vibao 200 - Babalevo

Babalevo amesema kwamba EP ya Diamond ilichaguliwa kutoka kwa vibao 200.

image
na Radio Jambo

Habari14 March 2022 - 05:56

Muhtasari


• Msanii Babalevo ameweka wazi kwamba EP yake Diamond Platinumz ilitokana na asilimia ndogo tu ya vibao zaidi ya 200 ambavyo mwanamuziki huyo bado hajaachia.

• Alitaja kwamba Simba ni msanii mkubwa ambaye amechangia pakubwa katika harakati za kukuza muziki wa Bongo, na kwamba anapaswa kupewa heshima yake.

 

Instagram, KWA HISANI

Msanii Babalevo ameweka wazi kwamba EP yake Diamond Platinumz ilitokana na asilimia ndogo tu ya vibao zaidi ya 200 ambavyo mwanamuziki huyo bado hajaachia.

Akizungumza katika mahojiano na Samissago, Babalevo alikiri kwamba hicho kilikuwa kionjo cha kazi nyingi ambazo Simba atakuwa anatoa.

“Hiyo EP ya FOA imetolea kwa nyimbo 200 alizonazo. Amezichambua akaona hizi acha niwapelekee mashabiki wangu,” alisema Babalevo.

Aidha Babalevo alisema kwamba atakuwa akiwaelezea mashabiki kila hatua ya maisha ya Diamond Platinumz kama njia moja ya kuonyesha kwamba yeye ni msanii mkubwa kupitia mambo anayoyafanya.

Aliongezea kwamba tayari Diamond alikuwa katika taifa la Nigeria ambapo alirekodi video nne za muziki ambazo zipo nje ya EP.

Alitaja kwamba Simba ni msanii mkubwa ambaye amechangia pakubwa katika harakati za kukuza muziki wa Bongo, na kwamba anapaswa kupewa heshima yake.

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved