logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Erick Omondi amzindua Wanjigi kuwania urais

Mcheshi Erick Omondi amemzindua Wanjigi kuwania urais katika uchaguzi ujao.

image
na Radio Jambo

Makala21 March 2022 - 05:57

Muhtasari


• Erick Omndi amesema kwamba Wanjigi ndiye chaguo bora la kuongoz ataifa hili.

• Alishikilia kwamba taifa linahitaji uongozi mpya ambao utawahudumia wananchi.

Instagram, KWA HISANI

Mcheshi Erick Omondi hatimaye amemzindua mfanyibiashara Jimmy Wanjigi kama mgombea faafu wa kiti cha urais katika uchaguzi wa Agosti 9.

Kupitia ujumbe aliochapisha katika ukurasa wake wa Instagram, Omondi alisema kwamba Wanjigi ndiye kiongozi ambaye anaweza kulikomboa taifa hili.

Omondi alisema kwamba Wanjigi ana maono makubwa ambayo yanaweza kubadilisha hali ya uchumi ya taifa hili.

Haya yanajiri wakati ambapo chama cha Safina ambapo Wanjigi ni mwanachama, kinatarajiwa kuandaa mkutano wa wajumbe wiki hii ili kujadili kuhusu mikakati yao mbele ya uchaguzi mkuu.

Ifahamike kwamba mcheshi huyo alikuwa ametoa siku saba kwa Ruto na Raila kumtafuta ili wafanye mazungumzo, la sivyo atachukua hatua ambayo itabadilisha siasa za Kenya na kuhakikisha wawili hao hawashindi uchaguzi.

Kwa muda sasa, amekuwa akiwarai vijana kuungana na kumchagua kiongozi anayefaa kwani wanajumuisha asilimia kubwa ya wapiga kura hivyo wanaweza kufanya uamuzi wa kiongozi atakayeingia madarakani.

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved