logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Usipofungua kioo watasema unaringa! Ankoo Zumoo amsuta shabiki aliyeiba miwani ya Irene Uwoya

Ankoo zumo ameonyesha kukasirishwa kwake baada ya shabiki kuiba miwani ya Uwoya.

image
na Radio Jambo

Habari21 March 2022 - 06:29

Muhtasari


• Ankoo Zumo ameonekana kukasirishwa na kitendo cha shabiki kuiba miwani ya mwanafilamu Irene Uwoya.

• Alisema kwamba mashabiki wanapaswa kutoa mazingira mazuri kwa wasanii wanapotangamana nao.

Instagram, KWA HISANI

Mwanafilamu kutoka Tanzania, Ankoo Zumo amemtupia vijembe shabiki ambaye alionekana akiiba miwani ya Irene Uwoya.

Kupitia aliyoipakia katika mtandao wake wa Instagram, shabiki huyo anaonekana akinyakua kwa nguvu miwani aliyokuwa ameivalia Uwoya.

Inasemekana Uwoya alikuwa katika harakati za kutangamana na mashabiki wake wakati kitendo hicho kilipotokea.

Kulingana na Zumo, hulka kama hizo ndizo zinazowafanya mastaa wengi kutotangamana kwa urais na mashabiki wao.

"Usipofungua kioo watasema unaringa, haya sasa kama hiyo miwani ilikuwa kwa ajili ya matatizo ya macho utamuuzia nani?" Zumo aliandika.

Baadhi ya mashabiki na wasanii walionekana kushangazwa na tukio hilo huku wakiwarai mashabiki kukoma hulka hizo.

Japo Uwoya hajazungumzia tukio hilo mpaka sasa, alionekana kukasirishwa nalo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved