logo

NOW ON AIR

Listen in Live

"Ni upuzi!" Bien awakemea wanaokejeli Kiingereza duni cha Diamond Platnumz

Bien amesema kwamba umahiri wa lugha ya Kiingereza sio kipimo cha akili.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri24 March 2022 - 10:28

Muhtasari


•Mbabe huyo wa muziki mwenye umri wa miaka 34 amesema kwamba umahiri wa lugha ya Kiingereza sio kipimo cha akili.

•Mwanamuziki huyo ameweka wazi kwamba atakapokuwa mzazi ni sharti atafunza watoto wake Kiluhya.

Bien na Diamond Platnumz

Mwanamuziki wa bendi ya Sauti Sol, Bien Aime Baraza amewakosoa wanamitandao wanaomkejeli Diamond Platnumz kwa kutokuwa na umahiri wa lugha ya Kiingereza. 

Akiwa kwenye mahojiano na Mpasho, Bien alisema kucheka Kingereza kibovu cha Diamond ni jambo la kipuzi na haifai.

"Hiyo ni upuzi! Huwa naona Wafaransa wanang'ang'ana kuzungumza Kizungu lakini huwa hamuwachekelei, Wajerumani vilevile huzungumza Kiiingereza kwa lafudhi. Watu wengi huzungumza Kiingereza kwa lafudhi, yamaanisha unajua lugha nyingine," Bien alisema.

Mbabe huyo wa muziki mwenye umri wa miaka 34 amesema kwamba umahiri wa lugha ya Kiingereza sio kipimo cha akili.

Alimpongeza sana Diamond kwa mafanikio makubwa ambayo ameweza kufanya katika taaluma yake ya usanii.

"Diamond ako na pesa. Anapiga kazi kabisa. Hao watu wanaandika vitu vya chuki nawaonea huruma tu," Alisema.

Bien alisema kwamba kujua lugha ya mama ni jambo muhimu sana. Aliweka wazi kwamba atakapokuwa mzazi ni sharti atafunza watoto wake Kiluhya.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved