logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Madaktari walitabiri ningekufa na miaka 15,' Akuku Danger azungumzia ugonjwa ambao amekua akipambana nao

Amesema huwa anakumbwa na uchungu mwingi kila mara ugonjwa huo unaposhambulia tena

image
na Radio Jambo

Habari28 March 2022 - 04:47

Muhtasari


•Mcheshaji huyo wa Churchill Show  alisema alikuja kufahamu kuhusu ugonjwa wake akiwa katika darasa la tano.

•Akuku amesema huwa anakumbwa na uchungu mwingi kila mara ugonjwa huo unaposhambulia tena. 

Mchekeshaji wa Churchill Show, Mannerson Oduor almaarufu Akuku Danger amefichua kuwa alizaliwa na ugonjwa wa Anemia ya Seli Mundu (Sickle-Cell anemia).

Akiwa kwenye mahojiano ya hivi majuzi na Mpasho, Akuku alieleza kwamba amekuwa akipambana na ugonjwa huo kwa miaka mingi

Mzaliwa huyo wa eneo la Nyanza  alisema alikuja kufahamu kuhusu ugonjwa wake akiwa katika darasa la tano.

"Nilipokuwa nakua nilikuwa naenda hospitalini mara kwa mara ili kuangaliwa. Kila mwezi lazima ningeenda hospitali. Haikuwa rahisi kwa sababu madawa yetu ni ghali," Akuku alisimulia.

Mchekeshaji huyo mwenye umri wa miaka 31 amefichua kwamba madaktari waliwahi kubashiri kuwa angeaga akiwa na miaka 15.

"Nilipokuwa na umri wa miaka 15, daktari aliniambia na mamangu tuende nyumbani nisubiri kufa. Akamwambia wamefanya kila wawezalo. Mama yangu alikuwa mtu wa dini hivyo aliendelea kuomba. Nilimwambia mama anipeleke nyumbani na nikaomba tumpigie simu mchungaji aje aniombee, nilikuwa na maumivu makali sana lakini sikuwa amini kuwa nitakufa," Akuku alisema.

Alifichua kwamba alikua na unyanyapa mwingi hasa alipokuwa katika shule ya msingi kwani hakuchukuliwa kama watoto wengine wa kawaida.

Akuku amesema huwa anakumbwa na uchungu mwingi kila mara ugonjwa huo unaposhambulia tena.  Mojawapo ya dalili ambazo humkumba ni kubadilika kwa rangi ya macho.

Hata hivyo ameweka wazi kwamba ugonjwa huo haumshtui tena kwani tayari amezoea kuishi nao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved