logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Hakuna mwanamke mzuri kama Hamisa Mobetto, Mwijaku ampa makavu Zuchu

Mwijaku amemtaka Zuchu kumlazimisha Diamond amuoe ili asije kujuta.

image
na

Habari31 March 2022 - 07:10

Muhtasari


• Mwijaku amesema kwamba hakuna mwanamke mrembo zaidi ya Hamisa Mobetto huko Tanzania.

• Amemtaka Zuchu kutojigamba sana kwa kuwa karibu na Diamond Platnumz.

Instagram, KWA HISANI

Mwanahabari kutoka Tanzania, Mwijaku amempa makavu Zuchu kwa kile anachokisema kwamba anavimba kutokana na ukaribu wake na Diamond Platnumz.

Akizungumza na mwanablogu mmoja, Mwijaku alimtaka Zuchu kufahamu  kwamba kulikuwa na wanawake warembo zaidi katika maisha ya Simba ila hawapo naye kwa sasa.

Mwijaku alimshauri Zuchu kumlazimisha Diamond Platnumz amuoe badala ya kuchezena.

Kauli hii ya Mwijaku ilijiri wakati ambapo pia  Khadija Kopa ambaye ni mamake Zuchu alitoa kauli tata akisema kwamba yeye ndiye amezaa mtoto ila wazazi wengine ashakum si matusi wamekunya.

Aidha, amesema kwamba Zuchu amefanya vizuri kimuziki ila bado ni mchanga kiakili na anapaswa kufanya maamuzi ya busara katika maisha yake.

Japo Zuchu na Diamond hawajaweka wazi  kwamba wanachumbiana, kuna ishara nyingi za wazi ambazo zinaonyesha pengine kuna kitu kinaendelea kati yao.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved