logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Harmonize amvulia kofia Eric Omondi, amtambua kama mchekeshaji mkubwa zaidi Afrika Mashariki

Alimtambulisha Eric kama nduguye mkubwa na mchekeshaji mkubwa zaidi Afrika Mashariki.

image
na Radio Jambo

Habari04 April 2022 - 18:30

Muhtasari


•Mwanamuziki huyo alimtambulisha Eric kama nduguye mkubwa na mchekeshaji mkubwa zaidi Afrika Mashariki.

•Eric ambaye alitimiza miaka 40 hivi majuzi amekuwa akijipiga kifua kuwa miongoni mwa wachekeshaji bora bara Afrika na kote Duniani.

Mchekeshaji mashuhuri aliyezingirwa na drama nyingi, Eric Omondi kwa sasa yupo nchini Tanzania kwa ziara ya kikazi.

Eric alitua katika nchi hiyo jirani siku ya Jumatatu na kupokewa na staa wa muziki wa Bongo, Harmonize.

Katika kanda ya video iliyopakiwa na Harmonize, wasanii hao wawili walioneka wakibarizi na kucheza mpira wa vikapu nyumbani kwa mmiliki huyo wa lebo ya Konde Gang. Mwanamuziki huyo alimtambulisha Eric kama nduguye mkubwa na mchekeshaji mkubwa zaidi Afrika Mashariki.

"Kaka yangu Eric Omondi, mchekeshaji mkubwa Afrika Mashariki alifika kijijini," Harmonize alisema kupitia ukurasa wake wa Instagram.

Eric ambaye alitimiza miaka 40 hivi majuzi amekuwa akijipiga kifua kuwa miongoni mwa wachekeshaji bora bara Afrika na kote Duniani.

Siku za hivi majuzi amejikita katika mstari wa mbele kupigania muziki wa Kenya huku akitaka uchezwe na ukubalike zaidi.



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved