logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Mungu akupe hitaji la moyo wako,'Ujumbe wa Lulu Hassan kwa Kanze Dena

Kwa upande wake Lulu alimwandikia ujumbe wa kipekee

image
na Radio Jambo

Habari12 April 2022 - 10:50

Muhtasari


  • Kanze Dena alikuwa mwanahabari mwenza wa Lulu kabla ya kupata wadhifa wa msemaji wa ikulu

Urafiki kati ya mwanahabari wa runinga ya Citizen Lulu Hassan na msemaji wa Ikulu Kane Dena umekuwa ukinoga kila kuchao.

Kanze Dena alikuwa mwanahabari mwenza wa Lulu kabla ya kupata wadhifa wa msemaji wa ikulu.

Huku Kanze akisherehekea siku yake ya kuzaliwa siku ya Jumanne wanamitandao walimtumia jumbe za kipekee alipokuwa akiadhimisha siku yake ya kuzaliwa.

Kwa upande wake Lulu alimwandikia ujumbe wa kipekee na kumtakia Mungu ampe hitaji la moyo wake.

"Happy Birthday dadaa mkubwa ,Mungu akupe hitaji la moyo wako ....❤❤ u dada mwenye roho yake @kanze_dena ..Uendelee kuwa baraka kwa wengi," Lulu Aliandika.

Mwanahabari huyo wa zamani wa Citizen TV alienda kwenye mitandao yake ya kijamii kusherehekea siku hii akisema anajivunia mwanamke ambaye amekuwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved