logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Diamond - Rihanna atakuwa kwenye albamu yangu, hii ama ile ijayo

Diamond Platnumz: Tumeshaongea Na Rihanna Na Timu Yake Na Kila Kitu Kipo Sawa

image
na Radio Jambo

Burudani21 April 2022 - 07:51

Muhtasari


• "Kwa Mambo Yanayoendelea Kwa Rihanna Sasa, Inaweza Ikafanya Akawepo Kwenye Album. Hii Au Ijayo,” - Diamond Platnumz

Rihanna, Diamond Platnumz

Nguli wa muziki wa kizazi kipya katika ukanda wa Afrika Mashariki Diamond Platnumz anasema ndoto yake kubwa ni kufanya collabo ya moto na msanii nguli kutoka Barbados, Rihanna.

Akizungumza katika mahojiano kupitia shirika la habari la BBC baada ya hafla ya kuizikiza miziki yake kwenye EP ya FOA, Diamond alisema analenga siku moja kabla hajaacha kufanya muziki awe amekipiga pamoja na Rihanna.

Msanii huyo aliwahakikishia mashabiki wake kote ulimwenguni kwamba tayari mazungumzo baina ya pande zote mbili yamefanyika kwa mafanikio makubwa na huenda akawepo kama si kwa albamu yake ya sasa basi kwenye albamu ijayo watamuona na kumsikia Rihanna akitema cheche kwenye spika pamoja na Diamond.

“Ningependa Kufanya Kazi Na Rihanna, nahisi itakuwa ni ngoma kali sana, Kama Sio Kwenye Album Hii Basi Album Yangu Inayofuata, Tumeshaongea Na Rihanna Na Timu Yake Na Kila Kitu Kipo Sawa, Kwa Mambo Yanayoendelea Kwa Rihanna Sasa, Inaweza Ikafanya Akawepo Kwenye Album. Hii Au Ijayo,” alisema Diamond kwa hakikisho kubwa kwa mashabiki wake.

Maneno haya ya Diamond yanawiana na maneno ambayo yalitamkwa na msalishaji wake wa muziki S2Kizzy ambaye alidokeza kwamba huenda akawa katika project moja na Rihanna na sasa wengi wanaamini huenda katika collabo hiyo, S2Kizzy ndiye atakuwa nyuma ya ujanja na mirindimo ya beats.

Kwa sasa Rihanna ni mjamzito ambapo hivi majuzi uvumi ulisambaa kwamba huenda wameachana na mpenzi wake msanii A$AP Rocky kwa kile kilisemekana kwamba ni mpenzi wake huyo kuchepuka na mwanadads anayemcvhagulia fasheni ya viatu Rihanna.

Ila madai haya yalipuuziliwa mbali muda mfupi baadae na rekodi lebo ya TMZ.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved