logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nitafurahi sana nikiwa na wapenzi 4-Mbosso

Kama Mwislamu, mwimbaji anaruhusiwa kuoa wake wanne.

image
na Radio Jambo

Yanayojiri11 May 2022 - 11:50

Muhtasari


  • Kama Mwislamu, mwimbaji anaruhusiwa kuoa wake wanne. Jumuiya za Kiislamu zinaruhusu hadi wake wanne

Mwimbaji wa Tanzania Mbosso amefunguka kuhusu jinsi angefurahi kuwa na wapenzi wanne.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, aliandika;

“Ukiwa na mpenzi mmoja anakupa furaha. Imagine ukiwa na wapenzi wanne hayo mafuraha yake," Aliandika Mbosso.

Si mara ya kwanza mwimbaji anazungumza kuhusu kuwa na wapenzi wengi. Mnamo 2020 alisema kuwa wake wanne hawatoshi, angependelea kuwa na wanawake 15 hadi 20.

Alisema hayo kwenye harusi ya Esma Platnumz;

"Wakati bachelors kama sisi wanaona tukio kama hili, inatupa msukumo wa kuoa. Nadhani pia nitapata wanawake warembo hapa, huwezi jua, naweza kupata mke hapa.”

"Kusema kweli, wake wanne hawatoshi, nikipata hata 20 au kumi au 15, nitakuwa mzuri. Lakini kwangu, wanawake wanne ni wachache sana.”

Kama Mwislamu, mwimbaji anaruhusiwa kuoa wake wanne. Jumuiya za Kiislamu zinaruhusu hadi wake wanne. Mbosso tayari ni baba wa watoto watatu kutoka kwa wanawake tofauti.

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved