logo

NOW ON AIR

Listen in Live

'Msinipigie simu usiku mkiwa mshaalewa,'Msanii Lady Jaydee awaonya watu wenye tabia hii

Usemi wa Lady Jaydee wa umri wa miaka 42 sasa unaonekana kukera watumizi wengi wa mitandao

image
na Radio Jambo

Yanayojiri25 May 2022 - 13:23

Muhtasari


  • Usemi wa Lady Jaydee wa umri wa miaka 42 sasa unaonekana kukera watumizi wengi wa mitandao ya kijamii hususan Twitter

Msanii kutoka Tanzania Lady JayDee kupitia kwenye ukurasa wake rasmi wa twitter amewaonya watu ambao wanatabia ya kumpigia simu usiku hasa wakati wamelewa.

KUlingana na msanii huyo watu hao hufanya hayo ili kijionyesha wako karibu naye, ilhali hawaungi mkono kazi yak.

"Watu mnaonifahamu msiwe mnanipigia simu usiku mkiwa mmeshalewa baada ya kusikia nyimbo zangu huko mlipo ili watu waone mna ukaribu na mimi wakati you don’t even support my businesses wala shows hamji. Kuweni outsiders tu siwa appreciate wala nini #FakeAss 😏," Msanii huyo Aliandika.

Usemi wa Lady Jaydee wa umri wa miaka 42 sasa unaonekana kukera watumizi wengi wa mitandao ya kijamii hususan Twitter.

Msanii huyo amekawia bila kuto kibao kipya, huku kibao cha mwisho akitoa akiwa amshirikiana na staa wa bongo Harmonize mwaka mmoja uliopita.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved